Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Sarah Obama afariki dunia, kuzikwa leo
Kimataifa

Sarah Obama afariki dunia, kuzikwa leo

Spread the love

 

SARAH Obama (99), Bibi wa Rais wa zamani wa Marekani, Barrack Obama, amefariki dunia leo Jumatatu tarehe 29 Machi 2021, katika Hospitali ya Jaramogi Oginga Odinga, Kisumu, nchini Kenya alipokuwa akipatiwa matibabu. Anaripoti mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Marsat Obama, mtoto wa Sara akizungumza na mtandao wa Daily Nation la Kenya amesema, mama yake amefariki alfajili ya saa 4:45, baada ya kufikishwa hospitalini hapo jana Jumapili kwa ajili ya matibabu.

Amesema, mama yake (Sarah), alikuwa mgonjwa wa kiharusi alichokipata kuanzia Septemba 2020 pamoja na kisukari.

Marsat amesema, mpango wa mazishi yanaendelea ambapo yanatarajiwa kufanyika leo Jumatatu au kesho katika makaburi ya Kiislamu yaliyopo Kisumu.

Kutokana na kifo hicho, Uhuru Kenyatta, Rais wa Kenya ametuma salamu za rambirambi kwa familia ya Obama akimwelezea Sarah alikuwa nembo ya familia na Kenya itaukumbuka mchango wake.

“Kifo cha Sarah ni pigo kwa taifa letu. Tumempoteza mtu muhimu, tunaungana na familia katika kipindi hiki kigumu wanachokipitia,” amesema Rais Kenyatta

Amesema, Sarah atakumbukwa kwa mchango wake hususan eneo la Nyang’oma Kagelo alipokuwa akifanya shughuli mbalimbali za kimaendeleo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!