Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu: Rais Magufuli amebakiza siku 14 Ikulu
Habari za SiasaTangulizi

Lissu: Rais Magufuli amebakiza siku 14 Ikulu

Spread the love

MGOMBEA Urais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amesema, Rais John Pombe Magufuli amebakisha siku 14 kubaki Ikulu, kwa kuwa hatoshinda katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Lissu ametoa kauli hiyo leo Jumatano tarehe 14 Oktoba 2020 wakati anazungumza na wananchi wa Kisiwa cha Ukerewe mkoani Mwanza, kuhusu changamoto wanazopitia kwenye sekta ya uvuvi katika mkutano wake wa kampeni.

Rais Magufuli anatetea kiti chake cha Urais kwa mara ya pili kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambapo aliingia madarakani tarehe 5 Novemba 2015 baada ya kushinda Uchaguzi Mkuu.

“Magufuli amebakisha wiki mbili Ikulu, tarehe 28 Oktoba 2020 tunawashinda, uchaguzi ukiisha hana kazi,” amesema Lissu.

Akizungumzia ahadi zake, Lissu amesema akichaguliwa kuwa Rais wa Tanzania, manyanyaso dhidi ya wananchi hasa wavuvi yatakuwa mwisho.

Amesema, ataunda tume itakayohusisha majaji wa mahakama za juu kuchunguza matukio ya unyanyasaji dhidi ya wavuvi.

“Jambo la kwanza kabisa kuhusiana na hili, kama rais wenu nitaunda tume ya majaji wa mahakama za juu kuchunguza matukio yote ya kuumiza watu, ya kutia watu umasikini ambayo yamefanyika katika mwambao wa Ziwa Victoria, Tanganyika na Nyasa. Sababu kote nilipopita wavuvi ni kilio kikubwa,”amesema Lissu.

Lissu amesema, lengo la uundwaji wa tume hiyo ni kufahamu watu waliohusika na matukio ya unyanyasaji wa wavuvi, kwa ajili ya kuwachukulia hatua waliohusikanayo.

Pia, Lissu ameahidi kuziboresha sheria za uvuvi, kupanua bandari ya Nansio Ukerewe pamoja na kujenga daraja litakalounganisha kisiwa cha Kisorya mkoani Mara na Ukerewe mkoani Mwanza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

Habari za SiasaTangulizi

Kinana: Hatukubali kushutumiwa kwa uongo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana amesema viongozi wa...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

error: Content is protected !!