Tuesday , 3 October 2023
Home Kitengo Michezo Ligi Kuu VPL kurejea tena leo
Michezo

Ligi Kuu VPL kurejea tena leo

Uhefu FC
Spread the love

LIGI kuu soka Tanzania Bara inaendelea tena leo kwa kupigwa jumla ya michezo minne katika viwanja tofauti mara baada ya mapumziko ya michezo ya kirafiki na kimashindano ya kalenda ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani ‘Fifa.’ Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mchezo wa mapema leo utawakutanisha JKT Tanzania ambao watakuwa nyumbani dhidi ya Ruvu Shooting, mechi itakayochezwa majira ya saa 8 mchana kwenye Uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma.

Mechi nyingine tatu zitachezwa majira ya saa 10 kamili jioni, ambapo KMC watawakaribisha Coastal Union kwenye Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam na Biashara United atakuwa kwenye dimba la Karume mkoni Mara kuwaalika Ihefu FC kutoka Mbeya.

KMC

Baada ya kupoteza dhidi ya Azam FC, klabu ya Kagera Sugar itakuwa na wakati wa kujiuliza mbele ya Namungo FC kwenye mchezo utakaochezwa kwenye Uwanja wa Majaliwa, Luangwa mkoani Lindi.

Mpaka ligi hiyo inasimama Azam FC walikuwa juu kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 15 huku nafasi ya pili ikishikwa na Simba yenye pointi 13 sawa na Yanga aliyeshika nafasi ya tatu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

UEFA imekuja na maokoto yakutosha bashiri na Meridianbet sasa

Spread the love UTAMU wa kubeti ule bhana, na ukitaka kula ni...

BiasharaMichezo

BetPawa kuwasaidia Watanzania 20 awamu ya 2 ‘Dream Maker’

Spread the loveKAMPUNI  ya michezo ya kubahatisha ya BetPawa Tanzania,  jana Jumatatu...

Michezo

Taswa wampongeza Mobhare Matinyi

Spread the love  CHAMA cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA),...

Michezo

Waziri madini atembelea banda la GGML, ashuhudia mradi wa uwanja wa kisasa

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde ametembelea banda la Kampuni ya...

error: Content is protected !!