Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa NEC yaamua rufaa 60, Jesca arejeshwa kumvaa Dk. Mwigulu
Habari za Siasa

NEC yaamua rufaa 60, Jesca arejeshwa kumvaa Dk. Mwigulu

Jesca Kishoa
Spread the love

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) nchini Tanzania, imemrejesha Jesca Kishoa kuwa mgombea ubunge Iramba Magharibi Mkoa wa Singida kupitia Chadema. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Jesca aliyekuwa mbunge wa viti maalum, atachuana na wagombea wa vyama vingine akiwemo Dk. Mwigulu Nchemba wa CCM.

Uamuzi uliotolewa jana Ijumaa tarehe 11 Septemba 2020 na Mkurugenzi wa Uchaguzi, Dk. Wilson Mahera ilisema tume hiyo ilizipitia, kuchambua na kuzifanyia uamuzi rufaa 60 kati ya hizo, mbili za wabunge na 58 za udiwani.

          Soma zaidi:-

Dk. Mahera alisema, “imekubali rufaa moja na kumrejesha mgombea katika orodha ya wabunge. Rufaa hiyo ni kutoka jimbo la Iramba Magharibi.”

Ingawa taarifa hiyo ya Dk. Mahera kutomtaja jina la mgombea lakini Jecsa mwenyewe aliandika kwenye kwenye ukurasa wake wa Twitter akishukuru kwa uamuzi huo wa NEC.

“Nashukuru Mungu kwa hili, sasa kazi ni moja tu, kulikomboa jimbo la Iramba,” aliandika Jesca ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Baraza la Wanawake wa Chadema-Bara (Bawacha).

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Dk. Wilson Mahera

Katika uamuzi mwingine, Dk. Mahera alisema Tume imekataa rufaa moja ya mgombea ubunge wa Iramba Magharibi ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.

Dk. Mahera alisema, Tume ilizipitia, kuzichambua na kuzifanyia uamuzi rufaa 58 za madiwani kati ya hizo 34 imezikubali na kuwarejesha wagombea katika orodha ya wagombea udiwani huku ikizikataa rufaa 23 za wagombea.

Taarifa yote ya Dk. Mahera hii hapa chini;

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

error: Content is protected !!