Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Milioni 4.9 zamkamatisha kigogo wa Takukuru
Habari Mchanganyiko

Milioni 4.9 zamkamatisha kigogo wa Takukuru

Afisa Uhusiano wa Takukuru, Doreen Kapwani
Spread the love

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) nchini Tanzania, imemkamata ofisa wake wa uchunguzi mwandamizi, Nina Sipilon Saibul kwa tuhuma za kuomba na kupokea rushwa ya Sh.4.9 milioni. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kinondoni … (endelea).

Taarifa iliyotolewa jana Ijumaa tarehe 11 Septemba 2020 na Doreen Kapwani, Ofisa Uhusiano wa Takukuru imesema, Nina alikamatwa jana Alhamisi.

Doreen alisema, Nina ambaye ni Afisa Uchunguzi ofisi ya Takukuru Kinondoni jijini Dar es Salaam, aliomba rushwa kutoka kwa mfanyabiashara mmoja wa Jiji hilo anayejishughulisha na shughuli za Real Estate.

“Takukuru Mkoa wa Kinondoni, ilipokea taarifa za malalamiko dhidi ya afisa wake, kuomba rushwa ili asiendelee na uchunguzi uliodaiwa ulikuwa ukiendelea ndani ya Takukuru dhidi ya mfanyabiashara huyo(mlalamikaji).”

“Baada ya taarifa hizo kupokelewa, uchunguzi wa awali wa kuthibitisha tuhuma hizo ulifanyika na kubaini upo ukweli wa madai ya kuomba hongo lakini hakukuwa na jalada wala uchunguzi wowote uliokuwa ukiendelea dhidi ya mlalamikaji,” amesema Doreen.

Alisema, Takukuru imechukua hatua hii ili kuhakikisha inajisafisha dhidi ya watumishi wake wachache wenye tabia ovu zenye kukichafua chombo hicho.

“Uchunguzi dhidi ya tuhuma hii unakamilishwa ili kuweza kuwafikisha watuhumiwa mahakamani mapema iwezekanavyo,” alisema Doreen.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!