Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Milioni 4.9 zamkamatisha kigogo wa Takukuru
Habari Mchanganyiko

Milioni 4.9 zamkamatisha kigogo wa Takukuru

Afisa Uhusiano wa Takukuru, Doreen Kapwani
Spread the love

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) nchini Tanzania, imemkamata ofisa wake wa uchunguzi mwandamizi, Nina Sipilon Saibul kwa tuhuma za kuomba na kupokea rushwa ya Sh.4.9 milioni. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kinondoni … (endelea).

Taarifa iliyotolewa jana Ijumaa tarehe 11 Septemba 2020 na Doreen Kapwani, Ofisa Uhusiano wa Takukuru imesema, Nina alikamatwa jana Alhamisi.

Doreen alisema, Nina ambaye ni Afisa Uchunguzi ofisi ya Takukuru Kinondoni jijini Dar es Salaam, aliomba rushwa kutoka kwa mfanyabiashara mmoja wa Jiji hilo anayejishughulisha na shughuli za Real Estate.

“Takukuru Mkoa wa Kinondoni, ilipokea taarifa za malalamiko dhidi ya afisa wake, kuomba rushwa ili asiendelee na uchunguzi uliodaiwa ulikuwa ukiendelea ndani ya Takukuru dhidi ya mfanyabiashara huyo(mlalamikaji).”

“Baada ya taarifa hizo kupokelewa, uchunguzi wa awali wa kuthibitisha tuhuma hizo ulifanyika na kubaini upo ukweli wa madai ya kuomba hongo lakini hakukuwa na jalada wala uchunguzi wowote uliokuwa ukiendelea dhidi ya mlalamikaji,” amesema Doreen.

Alisema, Takukuru imechukua hatua hii ili kuhakikisha inajisafisha dhidi ya watumishi wake wachache wenye tabia ovu zenye kukichafua chombo hicho.

“Uchunguzi dhidi ya tuhuma hii unakamilishwa ili kuweza kuwafikisha watuhumiwa mahakamani mapema iwezekanavyo,” alisema Doreen.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

Habari Mchanganyiko

Yara yaja na bima ya mazao kwa wakulima

Spread the love  WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...

error: Content is protected !!