TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) nchini Tanzani, imekubali rufaa 15 kati ya 55 za wagombea ubunge katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Taarifa ya Mkurugenzi wa Uchaguzi, Dk. Wilson Mahera aliyoitoa leo Jumanne tarehe 8 Septemba 2020 amesema, NEC imekataa rufaa 15 za wagombea ambao hawakuteuliwa.
Amesema, tume hiyo baada ya kuchambua rufaa hizo kwa kupitoa vielelezo mbalimbali imekataa rufaa 25 za kupinga kuteuliwa.
Dk. Mahera amesema, wahusika wa rufaa hizo, wameanza kupokea uamuzi kwa njia za barua.
Amesema, wanaendelea kuzipitia rufaa zote na watakuwa wakitoa taarifa kadri wanavyomaliza.
Uamuzi mzuri na ni kitu nilikitegemea kwa vyama hivi viwili Chadema na Act baada ya kifungu cha sheria kilichowabana kuungana siku 90 kabla ya uchaguzi kuanza
Kujaza fomu imekuwa sawa na mtihani wa shule? Ukikosea ndio basi? Hakuna kusahihisha makosa? DU