Monday , 6 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mwili wa Nkurunziza kuzikwa leo 
Kimataifa

Mwili wa Nkurunziza kuzikwa leo 

Mwili wa aliyekuwa Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza ukiagwa
Spread the love

SAFARI ya mwisho hapa duniani ya aliyekuwa Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza inahitimishwa leo Ijumaa tarehe 26 Juni 2020. Anaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea)

Mwili wa Nkurunziza aliyefariki dunia ghafla tarehe 8 Juni 2020 kwa shinikizo la damu unazikwa leo Ijumaa Mji wa Gitega katikati ya Burundi.

Nkurunziza alifikwa na mauti, ikiwa imesalia miezi miwili kukabidhi madaraka kwa Rais mteule wa wakati huo, Jenerali Evariste Ndayishimiye.

Kutokana na kifo hicho, Jenerali Ndayishimiye aliapishwa tarehe 18 Juni 2020 na leo anaongoza maelefu ya Warundi, wageni mbalimbali wa ndani nan je katika shughuli hiyo ya mwisho kwa mwili wa Nkurunziza.

Hadi anafikwa na mauti, Nkurunzinza alikuwa ameongoza Taifa hilo kwa miaka 15 kuanzia 2005-2020.

Nkurunziza hadi anafikwa na mauti alikuwa na miaka 55. Alizaliwa tarehe 18 Desemba 1964.

Kabla ya maziko, shughuli imeanza asubuhi katika uwanja wa mpira wa Ingoma mjini Gitega kisha mwili wake kupitishwa mbele ya wananchi watakaokuwa uwanjani humo kumwaga na baadae kufanyika maziko rasmi.

Baadhi ya wageni waliohudhuria ni Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa, Rais mstaafu wa Tanzania, Jakaya Kikwete na mkewe, Salima.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!