Sunday , 5 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CHAUMMA: Muafaka ni Tume Huru, Katiba Mpya
Habari za Siasa

CHAUMMA: Muafaka ni Tume Huru, Katiba Mpya

Hashim Rungwe, Mwenyekiti wa Chaumma
Spread the love

CHAMA cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), kimesema muarobaini wa dosari zilizojitokeza katika mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, ni Tume Huru na Katiba Mpya. Anaripoti Faki Sosi … (endelea). 

Hayo amesema Hashim Rungwe, Mwenyekiti wa CHAUMMA Taifa, leo tarehe 11 Novemba 2019 wakati akifanya mahojiano na MwanaHALISI ONLINE.

“Tuachiwe tufanye katiba mpya ya nchi tuondokane na mambo ya huyu mwenyekiti wa tume, hawa wote wanafuata amri ya serikali. Kwa sababu wanalipwa na serikali,  lazima wawe na upendeleo, ili wananchi wawe radhi, wafanye tume huru ya uchaguzi,” ameeleza Rungwe na kuongeza;

“Sisi tunataka tume huru ya uchaguzi ambayo sisi sote tutaenda kuilalamikia, sasa hivi sisi tutamlalamikia nani? Kama wanafanya vitu kinyume na sheria, haya mambo yanatia uchungu kwa nini wanatufanyia hivi, kama wao wameinunua nchi, wameinunua kwa bei gani?”

Rungwe amesema CHAUMMA hakitashiriki uchaguzi huo, hadi Tume Huru ya Uchaguzi.

“Mtazamo wa CHAUMMA ni kama tulivyoeleza, kwamba hakiungi mkono kuendelea na uchaguzi sababu tangu mwanzo umeonekana ni batili. CCM wamehodhi uchaguzi na watumishi wamekuwa upande wao. Umejawa ghiliba, haturudi kwenye uchaguzi hadi tume huru ipatikane, tume iliyopo ibadilishwe,” amesema Rungwe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!