Saturday , 4 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tume ya Uchaguzi yatangaza uchaguzi Jimbo la Nassari
Habari za SiasaTangulizi

Tume ya Uchaguzi yatangaza uchaguzi Jimbo la Nassari

Spread the love

MWENYEKITI wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Semistocles Kaijage ametangaza uchaguzi mdogo wa Jimbo la Arumeru Mashariki. Anaripoti Hamisi Mguta … (endelea).

Akitoa taarifa hiyo Jaji Kaijage amesema kuwa uchaguzi huo utafanyika tarehe 19, Mei 2019 na fomu za wagombea zitatolewa kati ya Aprili 15 au 19 na uteuzi wa wagombea utafanyika Aprili 19 mwaka huu.

“Kwa kuzingatia masharti ya vifungu vya 37 na 46 vya Sheria ya Uchaguzi tume inautaarifu Umma kuhusu ratiba ya uchaguzi wa jimbo hilo, kampeni za uchaguzi zitafanyika kati ya Aprili 29 hadi Mei 18, 2019 na siku ya uchaguzi itakuwa ni Mei 19”

Taarifa hii ya kufanyika kwa uchaguzi wa Jimbo la Arumeru inatokana na Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma kukubaliana na uamuzi wa Spika Ndugai kutangaza kuwa Joshua Nassari amepoteza sifa za kuwa Mbunge wa Jimbo hilo.

Nassari alivuliwa ubunge na Spika Ndugai Machi 14, 2019 kwa kilichodaiwa kuwa ni kutokana na kutohudhuria mikutano mitatu mfululizo bila taarifa rasmi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari MchanganyikoTangulizi

Usafiri baharini wasitishwa kukwepa athari za kimbunga Hidaya

Spread the loveUSAFIRI wa baharini umesimamishwa kwa muda ili kukwepa athari za...

error: Content is protected !!