RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Magufuli amemteua Adolf Ndunguru kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango anayeshughulikia Sera ambayo ilikuwa wazi. Anaripoti Hamis Mguta … (endelea).
Kabla ya uteuzi huo Nduguru alikuwa Naibu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ambapo kufuatia uteuzi huo Rais amemteua Msafiri Mbibo kuwa Naibu Kamishna Mkuu TRA.
Mbibo kabla ya kuteuliwa kwenye nafasi hiyo alikuwa Meneja wa TRA mkoa wa Kilimanjaro.
Kwa mujibu wa taatifa kutoka Ikulu iliyosainiwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu uteuzi huo unaanza mara moja leo Machi 31, 2019.
Leave a comment