Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Trump kupandishwa kizimbani
Kimataifa

Rais Trump kupandishwa kizimbani

Spread the love

RAIS wa Marekani, Donald Trump ameshtakiwa katika mahakama ya wilaya ya Kaskazini iliyoko kwenye jimbo la Calfornia, kwa kutangaza hali ya dharura ili akusanye fedha za ujenzi wa ukuta ulioko mpakani mwa taifa hilo na nchi ya Mexico. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Kesi hiyo imewasilishwa jana Jumatatu katika mahakama ya wilaya ya Kaskazini na muungano wa majimbo 16 ya nchini Marekani, yakiongoza na jimbo la Calfornia, ukiwa na lengo la kuiomba mahakama kuzuia matumizi mabaya ya nguvu za rais.

Mkuu wa Sheria katika jimbo la California, Xavier Becerra amedai kuwa, wanamshtaki Rais Trump ili kumzuia kutumia vibaya pesa za walipa kodi wa Marekani zilizotengwa kisheria na bunge kwa ajili ya matumizi ya watu walioko katika majimbo hayo 16.

Katika kesi hiyo, muungano huo umeiomba mahakama kutoa zuio kwa Rais Trump kutotekeleza mpango wake wa ujenzi wa ukuta hadi pale kesi itakapoanza kusikilizwa na kutolewa maamuzi.

Mwishoni mwa wiki iliyopita Rais Trump akiwa Ikulu ya ‘White House’ alitangaza hali ya hatari ili apate fursa ya kukusanya dola 8 bilioni kwa ajili ya kutekeleza ujenzi wa ukuta huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!