Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Magufuli: Lowassa ni ‘Super Man,’ wengine wataishia magerezani
Habari za SiasaTangulizi

Magufuli: Lowassa ni ‘Super Man,’ wengine wataishia magerezani

Spread the love

EDWARD Lowassa, Waziri Mkuu Mstaafu na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ametajwa kuwa ni miongoni mwa wanasiasa wanaofaa kuigwa. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa na Rais John Magufuli leo Jumanne tarehe 27 Novemba mwaka huu wakati wa ufungizi wa Maktaba mpya katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM).

“Maendeleo hayana chama, namwona Lowassa hapa naye yupo. Lowassa ni ‘Super Man’ ndio wanasiasa wanaofaa kuigwa. Wewe tumegombea nikakutupa nje lakini umekaa zako kimyaa. Tunahitaji wanasiasa wakomavu kama wewe,” amesema Rais Magufuli na kuongeza;

“Muda mrefu hatujaonana kwenye shuhuli kama hizi hapa. Nakupongeza sana. Naomba mumpigie makofi. Hii ndio Tanzania mpya, vyama vyetu visiwe chanzo cha vurugu. Wengine wanasema sema lakini hawakugombea. Yeye amekaa zake kimya.”

Hata hivyo, Rais Magufuli ameeleza kukasirishwa na wanasiasa ambao hawafuati sheria za nchi na kwamba, wataishia magerezani ili wakaheshimu sheria za nchi.

Miongoni mwa wanasiasa wakubwa wa upinzani nchini waliopo mahabusu gerezani Keko ni Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa na Ester Matiko ambaye ni Mbunge wa Tarime Mjini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

Habari za SiasaTangulizi

Kinana: Hatukubali kushutumiwa kwa uongo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana amesema viongozi wa...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

error: Content is protected !!