Sunday , 5 May 2024
Home Kitengo Michezo Tigo Fiesta yahairishwa
MichezoTangulizi

Tigo Fiesta yahairishwa

Spread the love

KAMATI ya Maandalizi ya Tamasha la Tigo Fiesta 2018 imesitisha tukio la kilele cha msimu wa tamasha hilo lililopaswa kufanyika leo tarehe 24 Novemba 2018. Anaripori Mwandishi Wetu … (endelea).

Tamasha hilo lilipaswa kufanyika kwenye viwanja vya Leaders vilivyopo Kinondoni jijini Dar es Salaam, lakini kamati hiyo kupitia taarifa yake iliyotoa leo, imesema imesitisha kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wake.

“Tunaomba radhi kwa madhara yoyote yatakayosababishwa na hili. Ambao walishanunua tiketi, kwa wale walionunua kupitia Tigo Pesa, fedha zao zitarejeshwa moja kwa moja kwenye simu zao kupitia mtandao, wlaionunua kwenye vituo vya mauzo wafike kwenye vituo wlaivyonunulia tiketi wakiwa na tiketi zao kwa ajili ya kurudishiwa fedha,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Kabla ya kamati hiyo kusitisha tamasha hilo, jana tarehe 23 Novemba 2018 Ofisi ya Afisa Utamaduni Manispaa ya Kinondoni ilitoa tamko la kusitisha kibali cha kufanyika tamasha hilo Leadres Club na kuhamishia katika uwanja wa uwanja wa Tanganyika Peackers ulioko Kawe.

Tamko hilo lilieleza kuwa, usitishaji huo unatokana na malalamiko ya baadhi ya wananchi na wagonjwa waliolazwa hospitalini kutokana na matangazo yanayoambatana na muziki unaopigwa kwa sauti kubwa katika tamasha hilo,na kuhatarisha afya za wagonjwa ikiwemo wa moyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Usiishie kuangalia tu game za leo, piga na mkwanja na Meridianbet

Spread the love  LIGI mbalimbali barani ulaya zitarejea tena Jumamosi ya leo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

error: Content is protected !!