Tuesday , 7 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mkuu wa Usalama Shirika la Posta atoweka kusikojulikana
Habari Mchanganyiko

Mkuu wa Usalama Shirika la Posta atoweka kusikojulikana

Spread the love

SHIRIKA la Posta Tanzania (TPC) linamsaka Mkuu wake wa Kitengo cha Usalama, George Mwamgabe anayedaiwa kutoweka kusiko julikana wiki moja iliyopita. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

TPC imefikia uamuzi huo baada ya Mwamgabe kutoonekana ofisini kwake kwa muda mrefu bila ya kutoa taarifa yoyote, ambapo ilimtafuta kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo nyumbani kwake pasipo mafanikio.

Taarifa ya TPC iliyotolewa na Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa shirika hilo, Joseph Ngowi imemtaka Mkuu huyo wa Usalama kuhudhuria kwenye kikao cha nidhamu kilichoitishwa, ambacho kinatarajiwa kufanyika tarehe 1 Novemba 2018 katika ofisi  za makao makuu ya TPC, kwa ajili ya kujibu tuhuma zinazomkabili.

Taarifa ya Ngowi inaeleza kuwa, kama Mwamgabe hatahudhuria kikao hicho pamoja na kutotoa taarifa kwa mwajiri wake, TPC itaendelea na kikao hicho ikiwemo maamuzi yake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

Habari Mchanganyiko

Mahakama yatoa uamuzi zuio dhidi ya Club House

Spread the loveMAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu jijini Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA yawanoa bodaboda 200 Arusha

Spread the loveZAIDI ya madereva bodaboda 200 wa jiji la Arusha wamepatiwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Serikali kuwakopesha wajasiriamali 18.5bn/- kupitia NMB

Spread the loveSerikali imetenga kiasi cha Sh 18.5 bilioni kwa ajili ya...

error: Content is protected !!