Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mkuu wa Usalama Shirika la Posta atoweka kusikojulikana
Habari Mchanganyiko

Mkuu wa Usalama Shirika la Posta atoweka kusikojulikana

Spread the love

SHIRIKA la Posta Tanzania (TPC) linamsaka Mkuu wake wa Kitengo cha Usalama, George Mwamgabe anayedaiwa kutoweka kusiko julikana wiki moja iliyopita. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

TPC imefikia uamuzi huo baada ya Mwamgabe kutoonekana ofisini kwake kwa muda mrefu bila ya kutoa taarifa yoyote, ambapo ilimtafuta kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo nyumbani kwake pasipo mafanikio.

Taarifa ya TPC iliyotolewa na Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa shirika hilo, Joseph Ngowi imemtaka Mkuu huyo wa Usalama kuhudhuria kwenye kikao cha nidhamu kilichoitishwa, ambacho kinatarajiwa kufanyika tarehe 1 Novemba 2018 katika ofisi  za makao makuu ya TPC, kwa ajili ya kujibu tuhuma zinazomkabili.

Taarifa ya Ngowi inaeleza kuwa, kama Mwamgabe hatahudhuria kikao hicho pamoja na kutotoa taarifa kwa mwajiri wake, TPC itaendelea na kikao hicho ikiwemo maamuzi yake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!