Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Tisa mbaroni kwa mauaji ya watoto wa familia moja
Habari Mchanganyiko

Tisa mbaroni kwa mauaji ya watoto wa familia moja

Pingu
Spread the love

JESHI la Polisi mkoani Kagera linawashikilia watu tisa wanaoshukiwa kuhusika na tukio la kuwauwa kinyama watoto wawili wa familia moja na kuwatupa kichakani kwenye kijiji cha Mashule wilaya ya Bukoba. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza na wanahabari mapema leo tarehe 23 Oktoba 2018, Kaimu Kamanda wa Polisi Kagera, Issack Msengi ameeleza kuwa, mauaji ya watoto hao, Auson Respikius (7) na Alistidia Respikius (5) yanahusishwa na imani za kishirikina.

“Mauaji haya ya watoto yanahusishwa na imani za kishirikina na mpaka sasa tunawashikilia watu Tisa kuhusiana na tukio hilo,” amesema Kamanda Msengi.

Kwa mujibu wa Baba wa watoto hao, John Respikius anadai kuwa watoto wake walipotea tangu Jumapili tarehe 21 Oktoba 2018 ambapo jana miili yao ilipatikana kichakani ikiwa imechinjwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tanzania  yasisitiza kuwa Kituo Kikuu cha Uchimbaji Madini Afrika

Spread the loveTanzania imeendelea kusisitiza adhma yake ya kuwa kituo kikuu cha...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Usafiri baharini wasitishwa kukwepa athari za kimbunga Hidaya

Spread the loveUSAFIRI wa baharini umesimamishwa kwa muda ili kukwepa athari za...

Habari Mchanganyiko

RPC Dodoma akabidhiwa bunduki mbili za wahalifu

Spread the love  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa ya Kulevya...

error: Content is protected !!