Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Tisa mbaroni kwa mauaji ya watoto wa familia moja
Habari Mchanganyiko

Tisa mbaroni kwa mauaji ya watoto wa familia moja

Pingu
Spread the love

JESHI la Polisi mkoani Kagera linawashikilia watu tisa wanaoshukiwa kuhusika na tukio la kuwauwa kinyama watoto wawili wa familia moja na kuwatupa kichakani kwenye kijiji cha Mashule wilaya ya Bukoba. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza na wanahabari mapema leo tarehe 23 Oktoba 2018, Kaimu Kamanda wa Polisi Kagera, Issack Msengi ameeleza kuwa, mauaji ya watoto hao, Auson Respikius (7) na Alistidia Respikius (5) yanahusishwa na imani za kishirikina.

“Mauaji haya ya watoto yanahusishwa na imani za kishirikina na mpaka sasa tunawashikilia watu Tisa kuhusiana na tukio hilo,” amesema Kamanda Msengi.

Kwa mujibu wa Baba wa watoto hao, John Respikius anadai kuwa watoto wake walipotea tangu Jumapili tarehe 21 Oktoba 2018 ambapo jana miili yao ilipatikana kichakani ikiwa imechinjwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

Habari Mchanganyiko

Yara yaja na bima ya mazao kwa wakulima

Spread the love  WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...

error: Content is protected !!