Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Prof. Ndalichako amuitia Takukuru mkuu wa chuo
Elimu

Prof. Ndalichako amuitia Takukuru mkuu wa chuo

Profesa Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu
Spread the love

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amemtaka Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Diwani Athuman kutuma wataalamu kuchunguza ujenzi wa baadhi ya majengo ya Chuo cha Ualimu Shinyanga (SHYCOM) pamoja na maafisa wa wizara yake waliosimamia ujenzi huo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Prof. Ndalichako ametoa agizo hilo alipotembelea chuoni hapo kwa ajili ya kukagua ujenzi huo, ambapo alikuta mkandarasi huyo hajakamilisha ujenzi wa majengo hayo tangu apewe kazi hiyo mwaka 2016.

Katika hatua nyingine, Prof. Ndalichako amemuagiza Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Profesa Sifuni Mchome kumuondoa Mkuu wa Chuo cha Ualimu Shinyanga (SHYCOM), Paschal Highmagway katika wadhifa wake baada ya kubaini kwamba ametoa taarifa za uongo kuhusu ujenzi huo.

Mkataba wa mkandarasi huyo ulitakiwa kuisha tarehe 5 Aprili 2018 lakini serikali ilimuongezea muda hadi Septemba 15 mwaka huu, lakini alishindwa kukamilisha ujenzi huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari Mchanganyiko

Chongolo aagiza TAKUKURU kuchunguza ujenzi wa bweni

Spread the loveMkuu wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amemuagiza Kamanda wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

Ugawaji taulo za kike watajwa kutokomeza utoro shuleni

Spread the loveBAADHI ya wanafunzi na walimu wa shule za sekondari mkoani...

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

error: Content is protected !!