Sunday , 2 April 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Marekani, Saudi Arabia watibuana
Kimataifa

Marekani, Saudi Arabia watibuana

Spread the love

MARAFIKI wawili, Taifa la Saudi Arabia na Marekani yameingia kwenye mgogoro. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kwa mujibu wa mtandao wa taarifa, Prince Salman ameishambulia Marekani kwa kusema kuwa, taifa la Saudi Arabia limekuwepo kwa miaka mingi kabla hata taifa la Marekani halijatengenezwa.

Na kwamba, Washington isiibabaishe Saudi Arabia yenye utajiri mkubwa wa mafuta.

Mwanamfalme wa Saudi Arabia ametoa maneno hayo baada ya Rais Donald Trump kutoa maneno ya kejeli kuhusu utawala wa Saudi Arabia kwamba hauna uhai bila taifa lake.

Mfalme Salman amesema, taifa la Saudi Arabia limekuwepo kwa miaka mingi kabla hata taifa la Marekani kuundwa hivyo Washington isiibabaishe Saudi Arabia yenye utajiri mkubwa wa mafuta.

Mwanamfalme amesema kuwa, nchi yake haitoilipa Washington kwa ajili ya usalama wake.

Majeshi ya Marekani ni sehemu muhimu ya ulinzi Saudi Arabia kwa muda mrefu sasa.

“Saudi Arabia imekuwepo kabla ya Marekani.Taifa la Saudi Arabia limekuwepo toka mwaka 1744 nikiamini ni miaka 30 kabla ya taifa la Marekani halijatengenezwa”,amesema Salman.

Wiki iliyopita rais Trump alisema kuwa mfalme wa Saudi Arabia hawezi kusalia madarakani kwa zaidi ya wiki mbili bila msaada wa jeshi la Marekani.

Salman nae ametoa jibu kwa tamko hilo na kusema kuwa mtu anapashwa kukubali kuwa kuna wakati rafiki anaweza kuzungumza vitu vizuri na wakati mwingine vitu vibaya.

“Kuna mikwaruzano kama hiyo hata ndani ya familia kwani hakuna rafiki atakaezungumza mambo mazuri kuhusu wewe kwa asilimia mia moja”,aliongeza Salman.

Salman amesisitiza kuwa Saudi Arabia imelipia tayari silaha zote ilizonunua kutoka Marekani na haitotoa hata senti moja kulipia ulinzi wa taifa lake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Marekani yatia mguu maaandamano Kenya, yatoa maagizo kwa Rais Ruto, Odinga

Spread the love  Mabalozi kutoka nchi sita za Magharibi, zikiongozwa na Marekani,...

Kimataifa

Papa Francis alazwa hospitali kutokana na maambukizi ya mapafu

Spread the love  KIONGOZI wa Kanisa katoliki duniani, Papa Francis jana Jumatano...

Kimataifa

Nyumba ya babu yake Makamu wa Rais wa Marekani yatafutwa Zambia

Spread the love  KAMALA Harris, makamu wa rais wa Marekani, amepanga kutembelea...

Kimataifa

Benki ya Uswizi mbioni kuziwekea vikwazo akaunti za siri za Wachina

Spread the love  WAKATI Serikali na Benki ya Uswizi ikichukua hatua kali...

error: Content is protected !!