Sunday , 2 April 2023
Home Kitengo Maisha Elimu Prof. Ndalichako amuitia Takukuru mkuu wa chuo
Elimu

Prof. Ndalichako amuitia Takukuru mkuu wa chuo

Profesa Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu
Spread the love

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amemtaka Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Diwani Athuman kutuma wataalamu kuchunguza ujenzi wa baadhi ya majengo ya Chuo cha Ualimu Shinyanga (SHYCOM) pamoja na maafisa wa wizara yake waliosimamia ujenzi huo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Prof. Ndalichako ametoa agizo hilo alipotembelea chuoni hapo kwa ajili ya kukagua ujenzi huo, ambapo alikuta mkandarasi huyo hajakamilisha ujenzi wa majengo hayo tangu apewe kazi hiyo mwaka 2016.

Katika hatua nyingine, Prof. Ndalichako amemuagiza Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Profesa Sifuni Mchome kumuondoa Mkuu wa Chuo cha Ualimu Shinyanga (SHYCOM), Paschal Highmagway katika wadhifa wake baada ya kubaini kwamba ametoa taarifa za uongo kuhusu ujenzi huo.

Mkataba wa mkandarasi huyo ulitakiwa kuisha tarehe 5 Aprili 2018 lakini serikali ilimuongezea muda hadi Septemba 15 mwaka huu, lakini alishindwa kukamilisha ujenzi huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari

Serikali yataka vijana  wajiunge na program atamizi ya biashara CBE

Spread the love  SERIKALI imewahamasisha vijana kujiunga na program atamizi inayotolewa na...

Elimu

Mfuko wa Jimbo Musoma Vijijini wamwaga mamilioni ujenzi maabara za sekondari

Spread the love  MFUKO wa Jimbo la Musoma Vijijini, Mkoa wa Mara,...

ElimuHabari

CBE yaanzisha Shahada 10 za Uzamili, CBE yajivunia wahitimu wanaoajirika

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimewataka wenye  kampuni na...

Elimu

Harambee ujenzi sekondari za Musoma Vijijini yashika kasi

Spread the love  HARAMBEE ya ujenzi na ukarabati wa shule za sekondari...

error: Content is protected !!