Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Prof. Ndalichako amuitia Takukuru mkuu wa chuo
Elimu

Prof. Ndalichako amuitia Takukuru mkuu wa chuo

Profesa Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu
Spread the love

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amemtaka Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Diwani Athuman kutuma wataalamu kuchunguza ujenzi wa baadhi ya majengo ya Chuo cha Ualimu Shinyanga (SHYCOM) pamoja na maafisa wa wizara yake waliosimamia ujenzi huo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Prof. Ndalichako ametoa agizo hilo alipotembelea chuoni hapo kwa ajili ya kukagua ujenzi huo, ambapo alikuta mkandarasi huyo hajakamilisha ujenzi wa majengo hayo tangu apewe kazi hiyo mwaka 2016.

Katika hatua nyingine, Prof. Ndalichako amemuagiza Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Profesa Sifuni Mchome kumuondoa Mkuu wa Chuo cha Ualimu Shinyanga (SHYCOM), Paschal Highmagway katika wadhifa wake baada ya kubaini kwamba ametoa taarifa za uongo kuhusu ujenzi huo.

Mkataba wa mkandarasi huyo ulitakiwa kuisha tarehe 5 Aprili 2018 lakini serikali ilimuongezea muda hadi Septemba 15 mwaka huu, lakini alishindwa kukamilisha ujenzi huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

error: Content is protected !!