Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Mtoto wa miaka mitano afariki kwa moto
Habari Mchanganyiko

Mtoto wa miaka mitano afariki kwa moto

Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza, ACP Jonathan Shanna
Spread the love

MTOTO wa miaka mitano, Solile Emannuel amefariki dunia katika ajali ya moto iliyotokea tarehe 3 Oktoba 2018 nyumbani kwao maeneo ya Nh’obola wilayani Nayamaga mkoa wa Mwanza. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza kuhusu tukio hilo leo tarehe 6 Oktoba 2018, Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza, ACP Jonathan Shanna amesema chanzo cha moto huo ni kuungua kwa godoro kulikosababishwa na marehemu alipokuwa anachezea njiti ya kiberiti.

Kamanda Shanna ameeleza kuwa, wakati mtoto huyo anafanya tukio hilo, aliachwa peke yake na wazazi wake waliokuwa bustanini wakilima.

“Tukio hilo limetokea tarehe 3 saa 17:00 jioni, wakati marehemu alipoachwa peke yake chumbani akila chakula huku wazazi wake wakiwa bustanini wakilima. Inadaiwa marehemu alikuwa akichezea njiti ya kiberiti na kupelekea kuwasha moto ulioanza kuunguza godoro, nguo na hatimaye kushika nyumba nzima hali iliyopelekea marehemu kukosa hewa na baadae kufariki dunia,” ameeleza Kamanda Shanna.

Amesema, baada ya tukio hilo kutokea, Jeshi la Polisi lilifika kwa haraka eneo la tukio na kushirkiana na wananchi kutoa msaada, lakini moto ulikuwa tayari umepoteza uhai wa mtoto na kutekeza mali na vitu vyote katika nyumba hiiyo.

“Thamani ya mali na vitu vilivyoteketea katika ajali hiyo bado haijafahamika. Mwili wa marehemu tayari umefanyiwa uchunguzi na kukabidhiwa kwa ndugu wa marehemu kwa ajili ya mazishi,” amesema.

Kufuatia tukio hilo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza, limewasisitiza wazazi na walezi kuwa waangalifu na watoto wakati wote, na waache tabia ya kuwaacha watoto kwenye nyumba peke yao kwani kunaweza kuhatarisha usalama wao na baadae kupata majeruhi au kufariki dunia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

Habari Mchanganyiko

Yara yaja na bima ya mazao kwa wakulima

Spread the love  WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...

error: Content is protected !!