Sunday , 5 May 2024
Habari za Siasa

Masikini Abdul Nondo!

Abdul Nondo, Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana ACT-Wazalendo
Spread the love

MAHAKAMA ya Mkoa wa Iringa imemkuta na kesi ya kujibu Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi nchini (TSNP) Abdul Nondo aliyeshitakiwa kwa madai ya kusambaza taarifa za uongo kwamba ametekwa. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Leo tarehe 27 Agosti 2018, Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo Liad Chamshama ametoa uamuzi huo kutokana na ushahidi uliowasilishwa mahakamani hapo na upande wa Jamhuri. Hakimu amemtaka Nondo andae utetezi wake.

Hakimu Chamshama amesema kuwa, kutokana na ushahidi uliowasilishwa na upande wa Jamhuri mahakama hiyo imemtaka Nondo kujibu tuhuma hizo.

Nondo ameshitakiwa mahakamani hapo kwa kosa la kusambaza taarifa za uongo kupita mtandao wa WhatsApp na kumdanganya Ofisa wa Polisi kwenye Kituo cha Polisi cha Mafinga.

Nondo alidaiwa kutenda kosa hilo tarehe 7 Machi mwaka huu akiwa eneo la Ubungo Jiji Dar es Salaam na Mafinga mkoani Iringa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

error: Content is protected !!