Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Lugola amweka ndani Mkuu wa kituo cha Polisi
Habari Mchanganyiko

Lugola amweka ndani Mkuu wa kituo cha Polisi

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kulia) akimuuliza maswali Mkuu wa Kituo cha Polisi Mtwara mjini, Ibrahim Mhando (kushoto) baada ya kushindwa kuwaweka mahabusu
Spread the love

KANGI Lugola Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, amemuweka ndani Ibrahim Mhando, Mkuu wa Kituo cha Polisi cha Kati mjini Mtwara (OCS) kwa kosa la kutowaweka mahabusu watu wanne wanaotuhumiwa kumpa taarifa ya uongo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Waziri Lugola ametoa agizo hilo asubuhi ya leo tarehe 27 Agosti, 2018 alipotembelea kituo hicho kwa kushtukiza, kwa ajili ya kuthibitisha utekelezwaji wa agizo lake alilolitoa jana la kuwekwa mahabusu Benjamin Kasiga Mhandisi Mshauri wa Kampuni ya Y&P Architects na wenzake kwa kosa la kutoa taarifa ya uongo kuhusu ujenzi wa Makao Makuu ya Uhamiaji Mtwara.

Alipotembelea kituo hapo, Waziri Lugola alimkuta Mhandisi Kasiga akiwa chumba cha upelelezi badala ya kuwekwa mahabusu ya polisi hiyo.

Kabla ya kuwekwa mahabusu, OCD Mhando alisema hakutekeleza agizo hilo kutokana na mahabusu ya kituo hicho kujaa watuhumiwa.

Hata hivyo, utetezi huo ulipingwa na Waziri Lugola akisema kuwa nafasi ya kukaa watuhumiwa ilikuwepo na kwamba wote wanne wangeweza kukaa bila tatizo lolote.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!