Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Jimbo la Same waahidiwa maji
Habari Mchanganyiko

Jimbo la Same waahidiwa maji

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Ramo Makani
Spread the love

SERIKALI imesema kutokana na changamoto ya upungufu wa maji katika Hifadhi ya Mkomazi inaendelea kuchimba mabwawa sita ili kukidhi mahitaji, anaandika Dany Tibason.

Hayo yameelezwa leo bungeni na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Ramo Makani alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Same Mashariki, Naghenjwa Kaboyoka (Chadema) ,ambaye alitaka kujua lini serikali itatatua kero ya maji katika eneo la hifadhi ya Mkomazi.

“Je ni lini Serikali itatengeneza miundombinu ya maji katika hifadhi ya Mkomazi ili kuzuia wanyamapori kuzurura kwenye makazi ya wananchi wakitafuta maji na kuharibu mazao yao,”?alihoji Kaboyoka.

Akijibu swali hilo, Makani amesema kutokana na changamoto ya upungufu wa maji serikali inaendelea kuchimba mabwawa sita ili kukidhi mahitaji hayo.

Amesema Bwawa moja lilikamilika katika mwaka wa fedha 2016-2017 na mengine matano yatachimbwa katika mwaka huu wa fedha 2017-2018.

Aidha, Naibu Waziri huyo amesema katika mwaka wa fedha 2017-2018, kisima kirefu kitachimbwa kwa ajili ya kusukuma maji na kujaza mabwawa yanayokauka ili kukidhi mahitaji ya maji wakati wa kiangazi kikali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tanzania  yasisitiza kuwa Kituo Kikuu cha Uchimbaji Madini Afrika

Spread the loveTanzania imeendelea kusisitiza adhma yake ya kuwa kituo kikuu cha...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Usafiri baharini wasitishwa kukwepa athari za kimbunga Hidaya

Spread the loveUSAFIRI wa baharini umesimamishwa kwa muda ili kukwepa athari za...

Habari Mchanganyiko

RPC Dodoma akabidhiwa bunduki mbili za wahalifu

Spread the love  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa ya Kulevya...

error: Content is protected !!