Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Jimbo la Same waahidiwa maji
Habari Mchanganyiko

Jimbo la Same waahidiwa maji

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Ramo Makani
Spread the love

SERIKALI imesema kutokana na changamoto ya upungufu wa maji katika Hifadhi ya Mkomazi inaendelea kuchimba mabwawa sita ili kukidhi mahitaji, anaandika Dany Tibason.

Hayo yameelezwa leo bungeni na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Ramo Makani alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Same Mashariki, Naghenjwa Kaboyoka (Chadema) ,ambaye alitaka kujua lini serikali itatatua kero ya maji katika eneo la hifadhi ya Mkomazi.

“Je ni lini Serikali itatengeneza miundombinu ya maji katika hifadhi ya Mkomazi ili kuzuia wanyamapori kuzurura kwenye makazi ya wananchi wakitafuta maji na kuharibu mazao yao,”?alihoji Kaboyoka.

Akijibu swali hilo, Makani amesema kutokana na changamoto ya upungufu wa maji serikali inaendelea kuchimba mabwawa sita ili kukidhi mahitaji hayo.

Amesema Bwawa moja lilikamilika katika mwaka wa fedha 2016-2017 na mengine matano yatachimbwa katika mwaka huu wa fedha 2017-2018.

Aidha, Naibu Waziri huyo amesema katika mwaka wa fedha 2017-2018, kisima kirefu kitachimbwa kwa ajili ya kusukuma maji na kujaza mabwawa yanayokauka ili kukidhi mahitaji ya maji wakati wa kiangazi kikali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!