Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Jimbo la Same waahidiwa maji
Habari Mchanganyiko

Jimbo la Same waahidiwa maji

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Ramo Makani
Spread the love

SERIKALI imesema kutokana na changamoto ya upungufu wa maji katika Hifadhi ya Mkomazi inaendelea kuchimba mabwawa sita ili kukidhi mahitaji, anaandika Dany Tibason.

Hayo yameelezwa leo bungeni na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Ramo Makani alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Same Mashariki, Naghenjwa Kaboyoka (Chadema) ,ambaye alitaka kujua lini serikali itatatua kero ya maji katika eneo la hifadhi ya Mkomazi.

“Je ni lini Serikali itatengeneza miundombinu ya maji katika hifadhi ya Mkomazi ili kuzuia wanyamapori kuzurura kwenye makazi ya wananchi wakitafuta maji na kuharibu mazao yao,”?alihoji Kaboyoka.

Akijibu swali hilo, Makani amesema kutokana na changamoto ya upungufu wa maji serikali inaendelea kuchimba mabwawa sita ili kukidhi mahitaji hayo.

Amesema Bwawa moja lilikamilika katika mwaka wa fedha 2016-2017 na mengine matano yatachimbwa katika mwaka huu wa fedha 2017-2018.

Aidha, Naibu Waziri huyo amesema katika mwaka wa fedha 2017-2018, kisima kirefu kitachimbwa kwa ajili ya kusukuma maji na kujaza mabwawa yanayokauka ili kukidhi mahitaji ya maji wakati wa kiangazi kikali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Vijana 400 waguswa na programu ya “Learning for Life” ya SBL

Spread the love  PROGRAMU ya “Learning for Life” imetimiza dhamira ya Serengeti...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

error: Content is protected !!