Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Machafuko yakosesha watoto elimu DRC 
Kimataifa

Machafuko yakosesha watoto elimu DRC 

Watoto nchini Kongo
Spread the love

ASASI isiyo ya kiserikali nchini kongo imesema  watoto wengi zaidi wanakosa elimu kutokana na mgogoro na mfumo duni wa elimu wa nchi hiyo. anaandika Victoria chance.

Ripoti ya Baraza la Wakimbizi la Norway imebainisha kuwa  asilimia 92 ya watoto wenye umri wa miaka sita hadi 11 wamekosa elimu katika miji iliyokumbwa na machafuko ya Kalemie na Tanganyika.

Shule 900 zimebomolewa kutokana na kushamiri kwa machafuko katika mkoa wa Kasai katikati mwa Kongo DRC katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

Asasi hiyo imetahadharisha pia kwamba nchi hiyo kubwa ya katikati mwa Afrika inakabiliwa na hatari ya kupoteza kizazi chake kijacho kwa sababu katika mwaka huu umetolewa mchango wa asilimia nne tu ya fedha za misaada ya kibinadamu kwa ajili ya sekta ya elimu ya Kongo DRC.

Baraza la Wakimbizi la Naorway limeongeza kuwa watoto waliotimiza umri wa kwenda shule wanachangia zaidi ya asilimia 17 ya watu wapatao milioni 3.8 waliopoteza makaazi yao nchini humo katika  kipindi cha miongo miwili iliyopita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!