Sunday , 2 April 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Machafuko yakosesha watoto elimu DRC 
Kimataifa

Machafuko yakosesha watoto elimu DRC 

Watoto nchini Kongo
Spread the love

ASASI isiyo ya kiserikali nchini kongo imesema  watoto wengi zaidi wanakosa elimu kutokana na mgogoro na mfumo duni wa elimu wa nchi hiyo. anaandika Victoria chance.

Ripoti ya Baraza la Wakimbizi la Norway imebainisha kuwa  asilimia 92 ya watoto wenye umri wa miaka sita hadi 11 wamekosa elimu katika miji iliyokumbwa na machafuko ya Kalemie na Tanganyika.

Shule 900 zimebomolewa kutokana na kushamiri kwa machafuko katika mkoa wa Kasai katikati mwa Kongo DRC katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

Asasi hiyo imetahadharisha pia kwamba nchi hiyo kubwa ya katikati mwa Afrika inakabiliwa na hatari ya kupoteza kizazi chake kijacho kwa sababu katika mwaka huu umetolewa mchango wa asilimia nne tu ya fedha za misaada ya kibinadamu kwa ajili ya sekta ya elimu ya Kongo DRC.

Baraza la Wakimbizi la Naorway limeongeza kuwa watoto waliotimiza umri wa kwenda shule wanachangia zaidi ya asilimia 17 ya watu wapatao milioni 3.8 waliopoteza makaazi yao nchini humo katika  kipindi cha miongo miwili iliyopita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Marekani yatia mguu maaandamano Kenya, yatoa maagizo kwa Rais Ruto, Odinga

Spread the love  Mabalozi kutoka nchi sita za Magharibi, zikiongozwa na Marekani,...

Kimataifa

Papa Francis alazwa hospitali kutokana na maambukizi ya mapafu

Spread the love  KIONGOZI wa Kanisa katoliki duniani, Papa Francis jana Jumatano...

Kimataifa

Nyumba ya babu yake Makamu wa Rais wa Marekani yatafutwa Zambia

Spread the love  KAMALA Harris, makamu wa rais wa Marekani, amepanga kutembelea...

Kimataifa

Benki ya Uswizi mbioni kuziwekea vikwazo akaunti za siri za Wachina

Spread the love  WAKATI Serikali na Benki ya Uswizi ikichukua hatua kali...

error: Content is protected !!