Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Vita vyapoteza watu 40 nchini Sudan
Kimataifa

Vita vyapoteza watu 40 nchini Sudan

Spread the love

WATU 40 wameuawa na kujeruhiwa katika mapigano mapya yaliyotokea katika jimbo la Yei nchini Sudan Kusini, anaandika Hellen Sisya.

Mapigano hayo ambayo yanatokana na mgogoro wa kisiasa nchini humo, yametokea kati ya jeshi la nchi hiyo pamoja na waasi wa taifa hilo.

Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, mpaka sasa  watu wengi wameuawa na kujeruhiwa  katika vita vinavyoendelea nchini humo na umezitaka pande kuu hasimu katika mgogoro huo  kufanya juhudi za kurejesha amani na maridhiano.

Sudan Kusini ilitumbukia katika machafuko na mapigano kati ya wafuasi wa Rais Salva Kiir na makamu wake wa zamani Riek Machar tangu mwaka 2013.

Salva Kiir alimtuhumu makamu wake huyo kwamba alipanga njama za kufanya mapinduzi.

Baada ya kushamiri kwa mgogoro huo na kwa juhudi mbalimbali za  kimataifa mwaka 2015 pande hizo mbili zilifikia makubaliano ya kugawana madaraka.

Hata hivyo, kukiukwa kwa vipengele vya makubaliano hayo, kulipelekea kuvunjika kwa makubaliano hayo na kwa mara nyingine nchi hiyo changa zaidi barani Afrika ikatumbukia katika vita na machafuko.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!