Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa China yajitosa kulinda amani Afrika
Kimataifa

China yajitosa kulinda amani Afrika

Meli ya kivita ya Kijeshi ya China
Spread the love

JESHI la China inajipanga kuweka kambi ya kijeshi nchini Djibouti huku lengo mojawapo likiwa ni kulinda amani kwa nchi za Afrika na Magharibi mwa Asia, anaandika Catherine Kayombo.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari China, tayari meli za kijeshi zimeondoka bandari ya Zhanjiang katika mkoa wa kusini wa Guangdong jana bila kutaja idadi ya wanajeshi au meli zilizopelekwa nchini humo kwa ajili ya kambi hiyo.

Kambi hiyo ambayo ni ya kwanza ya kigeni nchini Djibouti, itatumiwa kwa matumizi kadhaa ikiwemo kulinda amani barani Afrika na Magharibi mwa Asia, huduma za uokoaji, mazoezi ya kijeshi na kuimarisha ushikiano wa kijeshi baina ya nchi hizo mbili.

China imewekeza katika nchi za kiafrika na pia imeboresha kwa haraka jeshi lake miaka ya hivi karibuni. Kituo hicho cha Djibouti kimebuniwa kufuatiwa mazungumzo kati ya nchi hizo mbili na kinaonekana kama moja ya hatua ya China kuwa na mamlaka ya kijeshi nchini humo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!