JESHI la China inajipanga kuweka kambi ya kijeshi nchini Djibouti huku lengo mojawapo likiwa ni kulinda amani kwa nchi za Afrika na Magharibi mwa Asia, anaandika Catherine Kayombo.
Kwa mujibu wa Shirika la Habari China, tayari meli za kijeshi zimeondoka bandari ya Zhanjiang katika mkoa wa kusini wa Guangdong jana bila kutaja idadi ya wanajeshi au meli zilizopelekwa nchini humo kwa ajili ya kambi hiyo.
Kambi hiyo ambayo ni ya kwanza ya kigeni nchini Djibouti, itatumiwa kwa matumizi kadhaa ikiwemo kulinda amani barani Afrika na Magharibi mwa Asia, huduma za uokoaji, mazoezi ya kijeshi na kuimarisha ushikiano wa kijeshi baina ya nchi hizo mbili.
China imewekeza katika nchi za kiafrika na pia imeboresha kwa haraka jeshi lake miaka ya hivi karibuni. Kituo hicho cha Djibouti kimebuniwa kufuatiwa mazungumzo kati ya nchi hizo mbili na kinaonekana kama moja ya hatua ya China kuwa na mamlaka ya kijeshi nchini humo.
Leave a comment