Tuesday , 7 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mdee kutupwa mahabusu kwa saa 48
Habari za Siasa

Mdee kutupwa mahabusu kwa saa 48

Halima Mdee, Mbunge wa Kawe
Spread the love

ALLY Hapi, Mkuu wa Wilaya Kinondoni,  amemuagiza Suzan Kaganda, Kamanda wa Polisi  wa Kinondoni (RPC) kumkamata Halima Mdee, Mbunge wa Kawe kutokana na kutoa maneno ya uchochezi kwa Rais John Magufuli, anaandika Hamisi Mguta.

Hapi ametoa agizo hilo leo alipokuwa akizungumza na wanahabari ofisini kwake ambapo amemtaka RPC Kaganda kumweka mahabusu kwa saa 48.

Mdee anadaiwa kutoa maneno hayo ya kukashifu na ya uchochezi katika mkutano wake wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha) uliofanyika jana makao makuu ya chama hicho.

Hapi kuwa amesema kauli za Mdee kuhusu wanafunzi waliopata mimba kurudi shuleni, imemshtua yeye kama mwenyekiti wa  Kamati ya Ulinzi na Usalama wa wilaya hiyo.

“Maneno yake ni ya kichochezi ambayo hayakubaliki, hayafai kutolewa na kiongozi kama yeye hivyo namuagiza kamanda amkamate Mdee amweke ndani kwa saa 48 ili ahojiwe yale yote aliyoyaongea ili afikishwe kwenye vyombo vya usalama,”amesema.

Hata hivyo, Henry Kilewo amesema Mdee amekamatwa na Polisi na Kupekekwa kituoni Oysterbay.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Wanaotaka kujifunza ZEC kwao kukoje?

Spread the loveMKURUGENZI wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Thabit Idarous...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Biteko, Nape wanadanganya?

Spread the loveKWA mila na desturi zetu za Kiafrika mkubwa huwa hakosei,...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Miamka 60 ya Muungano: Tunakwama wapi?

Spread the loveRAIS wa Jamhuri, Samia Suluhu Hasssan, Ijumaa iliyopita, aliongoza mamilioni...

ElimuHabari za Siasa

Serikali kuongeza wanufaika mikopo ya elimu ya juu

Spread the loveSERIKALI imesema itaongeza idadi ya wanufaika wa mikopo ya elimu...

error: Content is protected !!