Saturday , 10 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mdee kutupwa mahabusu kwa saa 48
Habari za Siasa

Mdee kutupwa mahabusu kwa saa 48

Halima Mdee, Mbunge wa Kawe
Spread the love

ALLY Hapi, Mkuu wa Wilaya Kinondoni,  amemuagiza Suzan Kaganda, Kamanda wa Polisi  wa Kinondoni (RPC) kumkamata Halima Mdee, Mbunge wa Kawe kutokana na kutoa maneno ya uchochezi kwa Rais John Magufuli, anaandika Hamisi Mguta.

Hapi ametoa agizo hilo leo alipokuwa akizungumza na wanahabari ofisini kwake ambapo amemtaka RPC Kaganda kumweka mahabusu kwa saa 48.

Mdee anadaiwa kutoa maneno hayo ya kukashifu na ya uchochezi katika mkutano wake wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha) uliofanyika jana makao makuu ya chama hicho.

Hapi kuwa amesema kauli za Mdee kuhusu wanafunzi waliopata mimba kurudi shuleni, imemshtua yeye kama mwenyekiti wa  Kamati ya Ulinzi na Usalama wa wilaya hiyo.

“Maneno yake ni ya kichochezi ambayo hayakubaliki, hayafai kutolewa na kiongozi kama yeye hivyo namuagiza kamanda amkamate Mdee amweke ndani kwa saa 48 ili ahojiwe yale yote aliyoyaongea ili afikishwe kwenye vyombo vya usalama,”amesema.

Hata hivyo, Henry Kilewo amesema Mdee amekamatwa na Polisi na Kupekekwa kituoni Oysterbay.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lussu: Mkataba wa DP bandarini si wa miaka 100

Spread the loveMAKAMU Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, amesema hakuna ukweli wowote...

Habari za SiasaTangulizi

Maulid Mtulia: Kutoka ubunge hadi U-DAS

Spread the love ALIYEKUWA mbunge wa Kinondoni, kupitia vyama vya The Civil...

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

error: Content is protected !!