Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mdee kutupwa mahabusu kwa saa 48
Habari za Siasa

Mdee kutupwa mahabusu kwa saa 48

Halima Mdee, Mbunge wa Kawe
Spread the love

ALLY Hapi, Mkuu wa Wilaya Kinondoni,  amemuagiza Suzan Kaganda, Kamanda wa Polisi  wa Kinondoni (RPC) kumkamata Halima Mdee, Mbunge wa Kawe kutokana na kutoa maneno ya uchochezi kwa Rais John Magufuli, anaandika Hamisi Mguta.

Hapi ametoa agizo hilo leo alipokuwa akizungumza na wanahabari ofisini kwake ambapo amemtaka RPC Kaganda kumweka mahabusu kwa saa 48.

Mdee anadaiwa kutoa maneno hayo ya kukashifu na ya uchochezi katika mkutano wake wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha) uliofanyika jana makao makuu ya chama hicho.

Hapi kuwa amesema kauli za Mdee kuhusu wanafunzi waliopata mimba kurudi shuleni, imemshtua yeye kama mwenyekiti wa  Kamati ya Ulinzi na Usalama wa wilaya hiyo.

“Maneno yake ni ya kichochezi ambayo hayakubaliki, hayafai kutolewa na kiongozi kama yeye hivyo namuagiza kamanda amkamate Mdee amweke ndani kwa saa 48 ili ahojiwe yale yote aliyoyaongea ili afikishwe kwenye vyombo vya usalama,”amesema.

Hata hivyo, Henry Kilewo amesema Mdee amekamatwa na Polisi na Kupekekwa kituoni Oysterbay.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!