Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo Simba, Yanga hapatoshi Mapinduzi Cup
Michezo

Simba, Yanga hapatoshi Mapinduzi Cup

Wachezaji wa Simba na Yanga wakiingia uwanjani katika moja ya pambano lao
Spread the love

HATIMAYE mahasimu wa wawili katika soka la Tanzania, Simba na Yanga wataminyana kesho katika hatua ya nusu fainali kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi inayoendelea visiwani Zanzibar baada ya kukamilika kwa michezo ya hatua ya makundi jana.

Simba wanakutana na Yanga baada ya kufanikiwa kumaliza vinara katika kundi A huku nafasi ya pili ikishikwa na timu ya Taifa Jang’ombe ambao walifanikiwa kupata ushindi jana mbele ya mabingwa watetezi URA kutoka nchini Uganda.

Katika mchezo huo utakaopigwa kesho majira ya Saa 2:15 usiku Yanga inaingia uwanjani ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza kataika mchezo uliomalizika dhidi ya Azam FC baada ya kupata kipigo cha mabao 4-0.

Mchezo wa pili wa nusu fainali utaikutanisha klabu ya Azam FC dhidi ya timu ya Taifa Jang’ombe ambayo ndio timu pekee kutoka visiwani humo kufikia hatua hiyo katika michuano hiyo inayotalajia kukamilika tarehe 12.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!