Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Simba, Yanga hapatoshi Mapinduzi Cup
Michezo

Simba, Yanga hapatoshi Mapinduzi Cup

Wachezaji wa Simba na Yanga wakiingia uwanjani katika moja ya pambano lao
Spread the love

HATIMAYE mahasimu wa wawili katika soka la Tanzania, Simba na Yanga wataminyana kesho katika hatua ya nusu fainali kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi inayoendelea visiwani Zanzibar baada ya kukamilika kwa michezo ya hatua ya makundi jana.

Simba wanakutana na Yanga baada ya kufanikiwa kumaliza vinara katika kundi A huku nafasi ya pili ikishikwa na timu ya Taifa Jang’ombe ambao walifanikiwa kupata ushindi jana mbele ya mabingwa watetezi URA kutoka nchini Uganda.

Katika mchezo huo utakaopigwa kesho majira ya Saa 2:15 usiku Yanga inaingia uwanjani ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza kataika mchezo uliomalizika dhidi ya Azam FC baada ya kupata kipigo cha mabao 4-0.

Mchezo wa pili wa nusu fainali utaikutanisha klabu ya Azam FC dhidi ya timu ya Taifa Jang’ombe ambayo ndio timu pekee kutoka visiwani humo kufikia hatua hiyo katika michuano hiyo inayotalajia kukamilika tarehe 12.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

error: Content is protected !!