Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo Yanga, Simba wang’ara kimataifa
MichezoTangulizi

Yanga, Simba wang’ara kimataifa

Spread the love

WATANI wa jadi Simba na Yanga wameanza vema kuipeperusha bendera ya Tanzania kimataifa baada ya kuibuka na ushindi mnono ugenini katika raundi ya awali ya Ligi ya mabingwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Yanga waliokuwa katika uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar es Salaam ambao umetumiwa na Klabu ya Zalan kutoka Sudan Kusini kama uwanja wao wa nyumbani, wameibuka na ushindi wa mabao 4 kwa nunge.

Mabao ya Yanga yamewekwa nyavuni na kiungo wao Feisall Salumu ‘Feitoto’ na mshambuliaji wao matata, Fiston Mayele aliyeondoka na mpira baada ya kupiga hattrick.

Aliyefungua karamu ya mabao alikuwa Mayele dakika ya 47, Feitoto dakika ya 54 kisha Mayele akamalizia misumari dakika ya 84 na 87.

Licha ya Yanga kupata ushindi huo, Zalan waliokolewa na golikipa wao baada ya kuokoa mashuti nane yaliyolenga lango katika kipindi cha kwanza na kuwafanya Yanga waende kujiuliza vyumbani katika dakika hizo 45 kabla ya kurejea na moto mkali.

Kwa upande wa Simba SC. ambao walikuwa ugenini nchini Malawi kupepetana na Nyasa Big Bullet, nao waliwatungua wenyeji hao bao 2-0.

Mabao ya Simba yamewekwa kambani na Moses Phiri dakika ya 29 na John Bocco dakika 84 na kuwafanya wekundu hao wa Msimba kurejea na matumaini tele nyumbani.

Kwa matoke hayo, timu hizo zimejiweka katika nafasi nzuri ya kuingia kwenye raundi ya kwanza katika Ligi hiyo ya Mabingwa Afrika baada ya kurejea wikiendi ijayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

Habari MchanganyikoTangulizi

Walimu 5000 Songwe waililia CWT kuwanyima sare

Spread the loveZaidi ya walimu 5000 ambao ni wanachama wa Chama cha...

error: Content is protected !!