Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa harles III athibitishwa kuwa mfalme Uingereza
Kimataifa

harles III athibitishwa kuwa mfalme Uingereza

Mfalme Charles III
Spread the love

 

BARAZA la Kukabidhi Mamlaka la Uingereza, limetangaza rasmi mtoto wa kwanza wa Malkia Elizabeth II, Charles Philip Arthur George, kuwa mfalme wa taifa hilo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Charles atakayefahamika kwa jina la Mfalme Charles III, amekabidhiwa mamkala hayo rasmi leo Jumamosi, tarehe 10 Septemba 2022, na Karani wa baraza hilo la siri, Richard Tilbrook, kuwa mfalme wa Uingereza, kiongozi wa Jumuiya ya Madola na mlinzi wa imani.

Baraza hilo la siri limemtangaza ikiwa ni siku moja tangu mama yake, Malkia Elizabeth afariki dunia Alhamisi iliyopita, nchini Scotland alikokuwa anapatiwa matibabu.

Baada ya kutangazwa kushika wadhifa huo, Mfalme Charles ameahidi kuliongoza taifa hilo kwa kufuata nyayo za marehemu mama yake aliyeiongoza Uingereza kwa miaka 70.

Aidha, Mfalme Charles amewashukuru watu ulimwenguni kote waliotuma salamu za rambirambi kwa familia yake kufuatia kifo cha mama yake Malkia Elizabeth.

Hafla hiyo iliyofanyika katika kasri la St. James, jijini London, imehudhuriwa na watu mbalimbali, wakiwemo wanafamilia ya kifalme, Waziri Mkuu wa Uingereza, Liz Truss.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!