Waziri Mkuu wa Palestina, Mohammed Shtayyeh ametangaza kujiuzulu pamoja na serikali yake katika hatua ambayo huenda ikafungua njia ya mageuzi yanayoungwa mkono na Marekani. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Uamuzi huo wa kujiuzulu kwa Shtayyeh lazima ukubaliwe Rais Mahmoud Abbas kabla ya kutekelezwa kwake.
Hatua hiyo inaashiria nia ya uongozi huo wa Palestina unaoungwa mkono na nchi za Magharibi kukubali mabadiliko ambayo yanaweza kuleta mageuzi yanayoonekana kuwa muhimu katika kuifufua serikali ya Mamlaka ya Palestina.
Marekani inataka serikali ya Palestina iliyofanyiwa mageuzi kuutawala Ukanda wa Gaza mara baada ya kumalizika kwa
vita vya Israel kwenye Ukanda huo, lakini bado kuna vikwazo vingi katika kutimiza matakwa hayo.
Leave a comment