Wednesday , 8 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Waziri Aweso aeleza mikakati kumaliza mgawo wa maji Dar
Habari Mchanganyiko

Waziri Aweso aeleza mikakati kumaliza mgawo wa maji Dar

Waziri wa Maji, Jumaa Aweso
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imepanga kutumia zaidi ya Sh.390 bilioni kujenga bwawa la kuhifadhia maji katika Kijiji cha Kidunda wilayani Morogoro vijijini mkoani Morogoro. Anaripoti Danson Kaijage, Morogoro … (endelea).

Ujenzi huo una lengo la kuweka akiba ya Mto Ruvu ambao ni chanzo kikubwa cha huduma ya Maji kwa mikoa ya Pwani na Dar es Salaam.

Bwawa hilo linategemea kuwa na urefu wa mita 860 na kimo cha mita 21 na uwezo wa kuhifadhi maji lita billioni 190.

Maji hayo kwa sehemu kubwa husababisha mafuriko wakati wa mvua za masika hivyo yakihifadhiwa kwenye bwawa hilo la yatasaidia tatizo la upatikanaji wa maji wakati wa kiangazi.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, mara baada ya kutembelea ili kuona na kujiridhisha eneo la utekelezaji wa mradi huo mkubwa wa kimkakati.

Mbele ya waandishi wa habari, Waziri Aweso amesema Serikali imeshalipa fidia ya Sh.12 billioni kwa wananchi wa eneo la Kidunda waliopisha ujenzi wa bwawa hilo na tayari wananchi wameshaondoka eneo la mradi ili kupisha ujenzi kuanza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

Habari Mchanganyiko

Mafunzo kwa bodaboda 395 yamkuna Meya Dodoma

Spread the loveNAIBU Meya wa Jiji la Dodoma, Asma Karama amepongeza mafunzo...

Habari Mchanganyiko

Samia aagiza huduma za dharura maeneo yaliyoathiriwa na kimbunga Hidaya

Spread the love   RAIS wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Samia...

error: Content is protected !!