Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Waziri Aweso aeleza mikakati kumaliza mgawo wa maji Dar
Habari Mchanganyiko

Waziri Aweso aeleza mikakati kumaliza mgawo wa maji Dar

Waziri wa Maji, Jumaa Aweso
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imepanga kutumia zaidi ya Sh.390 bilioni kujenga bwawa la kuhifadhia maji katika Kijiji cha Kidunda wilayani Morogoro vijijini mkoani Morogoro. Anaripoti Danson Kaijage, Morogoro … (endelea).

Ujenzi huo una lengo la kuweka akiba ya Mto Ruvu ambao ni chanzo kikubwa cha huduma ya Maji kwa mikoa ya Pwani na Dar es Salaam.

Bwawa hilo linategemea kuwa na urefu wa mita 860 na kimo cha mita 21 na uwezo wa kuhifadhi maji lita billioni 190.

Maji hayo kwa sehemu kubwa husababisha mafuriko wakati wa mvua za masika hivyo yakihifadhiwa kwenye bwawa hilo la yatasaidia tatizo la upatikanaji wa maji wakati wa kiangazi.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, mara baada ya kutembelea ili kuona na kujiridhisha eneo la utekelezaji wa mradi huo mkubwa wa kimkakati.

Mbele ya waandishi wa habari, Waziri Aweso amesema Serikali imeshalipa fidia ya Sh.12 billioni kwa wananchi wa eneo la Kidunda waliopisha ujenzi wa bwawa hilo na tayari wananchi wameshaondoka eneo la mradi ili kupisha ujenzi kuanza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NMB yakabidhi vifaa vya ujenzi, samani kwa shule ya msingi Sinyaulime, Chuo cha FDC Morogoro

Spread the loveBENKI ya NMB imekabidhi vifaa vya ujenzi kwa shule ya...

Habari Mchanganyiko

NMB Bonge la Mpango – ‘Moto Uleule’ yazinduliwa, Milioni 180…

Spread the loveMSIMU wa tatu wa Kampeni ya kuhamasisha utamaduni wa Kuweka...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

error: Content is protected !!