Saturday , 2 December 2023
Home Kitengo Michezo Wawa, Miquison warejea kikosini, Kuwavaa Namungo Jumapili
Michezo

Wawa, Miquison warejea kikosini, Kuwavaa Namungo Jumapili

Spread the love

WACHEZAJI wa klabu ya Simba, Pascal Wawa na Luis Miquison wamerejea leo kikosini kwa kuingia kambini baada ya kuwasili leo nchini kutoka kwenye nchi zao walipokuwa wameenda kimapumziko. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Wachechaji hao ambao wamerudi nchini leo mchana na watakuwa sehemu ya kikosi kitakachosafiri kwenda Jijini Arusha ambapo Simba itakuwa na mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Namungo FC, utakaochezwa kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

Wachezaji hao waliondoka nchini mara baada ya msimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2019/20 kumalizika na wote kwa nyakati tofauti walienda kufunga ndoa.

Miquison alifunga ndoa yake na mwenza wake tarehe 22 Agosti, 2020 kama taarifa kutoka kwenye uongozi wa klabu hiyo zilivyoeleza.

Taarifa za kurejea kwao zimetolewa kupitia kurasa za mitandao ya kijamii ya klabu hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Fernandes hakamatiki Man Utd, mahesabu ni kuifunga Bayern

Spread the love  NAHODHA wa Manchester United, Bruno Fernandes, alikuwa na kiwango...

Michezo

Meridianbet na Ligi ya Europa inakupa pesa za kumwaga mapema sana

Spread the love  KOMBE la UEFA Europa League ni zito kuliko makombe...

Michezo

Kwapua mpunga na mechi za UEFA leo na kesho

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya kuendelea leo na kesho...

AfyaMichezo

GGML yatoa milioni 17 kung’arisha ATF Marathon

Spread the loveKATIKA kuendelea kuunga mkono jitihada za Serikali kukabiliana na maambukizi...

error: Content is protected !!