Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Pogba aambukizwa corona, atoswa Ufaransa
KimataifaMichezo

Pogba aambukizwa corona, atoswa Ufaransa

Paul Pogba
Spread the love

PAUL Pogba, kiungo wa Manchester United, ameachwa katika kikosi cha Timu ya Taifa ya Ufaransa, baada ya kubainika kuambukizwa virusi vya corona (COVID-19). Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea)

Kikosi hicho cha Ufaransa kitacheza michezo miwili ya kirafiki na Sweden tarehe 5 Septemba 2020 na mchezo wa pili kitacheza nyumbani Paris 8 Septemba 2020.

Mchezaji mwingine ambaye ameachwa katika kikosi hicho baada ya kukutwa na  corona ni kiungo wa Tanguy Ndombele wa timu ya Tottenham Hotspur ya Uingereza.

Kocha wa timu hiyo, Didier Deschamps amesema, ameamua kufanya mabadiliko ya kumwita kikosini Eduardo Camavinga wa timu ya Rennes ya Ufaransa kuchukua nafasi ya Pogba ambaye jana alipimwa na kukutwa na corona.

Paul Pogba

Wawili hao wamelazimika kusalia Uingereza kwa mujibu wa taratibu, wanapaswa kujitenga kwa siku 14.

Hatua hiyo, inawafanya wachezaji hao kila mmoja kukosa maandalizi ya msimu wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) itakayoanza tarehe 12 Septemba 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!