Thursday , 9 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wanajeshi 7 wahukumiwa kifo kwa kukimbia maadui
Habari Mchanganyiko

Wanajeshi 7 wahukumiwa kifo kwa kukimbia maadui

Spread the love

WANAJESHI saba wa DR Congo wamehukumiwa kifo kwa kuonyesha uoga mbele ya wapiganaji wa kikundi cha waasi wa M23 na kukimbia hali inayodaiwa kuzidisha hofu kwa wananchi. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa …(endelea).

Mwendesha mashtaka wa kijeshi alisema tarehe 9 Februari 2023, wanajeshi hao walipitia katikati ya eneo la Sake, kilomita 25 magharibi mwa mji wa Goma uliopo mashariki mwa Kongo, wakipiga risasi kiholela walipokuwa wakiwakimbia waasi hao.

Hata hivyo, wanajeshi hao walikanusha mashtaka na mawakili wao walisema watakata rufaa dhidi ya uamuzi wa mahakama hiyo.

Mwendesha mashtaka alisema raia wawili waliuawa na wengine wanne kujeruhiwa vibaya wakati wa tukio hilo lililosababishwa na kitendo cha askari.

Maelfu ya watu hivi karibuni wamekimbia makazi yao hadi Goma na Minova huku waasi wa M23 wakikaribia mji huo kutoka eneo la Masisi magharibi.

Novemba mwaka jana, mahakama ya kijeshi ya Goma iliwahukumu kifo askari watatu kwa kukimbia vitani wakati wa makabiliano dhidi ya M23 na kusababisha hofu miongoni mwa raia.

Adhabu za kifo bado zinatolewa nchini DR Congo lakini mara ya mwisho zilitekelezwa mwaka 2003. Aidha, adhabu hizo zimeanza kubadilishwa taratibu na kuwa kifungo cha maisha.

1 Comment

  • Nawapa pole sana maskari hao kwa hukumu hiyo iliyotolewa,japo wamekiuka kiapo chao ila badala ya kifo basi wahukumiwe kifungo cha maisha

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali yapunguza kodi ya makampuni kwa 20%

Spread the loveSERIKALI imepunguza kodi ya makampuni kwa asilimia 20, kutoka asilimia...

Habari Mchanganyiko

Mradi uliotaka kumng’oa madarakani Dk. Mpango waanza majaribio

Spread the loveMRADI wa maji wa Mwanga-Same-Korogwe, ambao Makamu wa Rais, Dk....

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Madiwani Msalala wampa tano DED kwa kuongeza mapato

Spread the loveMKURUGENZI wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala, mkoani Shinyanga, Khamis...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kimbunga Hidaya chaua 5, kaya 7,027 zikikosa makazi

Spread the loveSERIKALI imetoa tathmini ya athari za kimbunga Hidaya, kilichotokea tarehe...

error: Content is protected !!