CHAMA cha Wakulima nchini (AAFP), kimesema kinamkumbuka aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, Hayati John Magufuli, kutokana na kazi kubwa aliyofanya kulinda demokrasia na kuwainua wakulima kwa kuondoa utitiri wa kodi zilizokuwa zinawakandamiza. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).
Kauli hiyo imetolewa leo Jumapili, tarehe 12 Februari 2023, na Mwenyekiti wa AAFP anayemaliza muda wake, Said Soud Said, katika mkutano mkuu wa chama hicho uliofanyika jijini Dar es Salaam.
“Nafungua mkutano huu kwa kumkumbuka hayati Magufuli, kutokana na uwanja wa demokrasia ambao kwa namna moja au nyingine aliwezssha kifikia hatua ya Tanzania kuwa nchi ya amani na utulivu,” amesema Said.
Mwenyekiti huyo wa AAFP, amemuomba Rais Samia Suluhu Hassan, kuendeleza yale mema yaliyoachwa na mtangulizi wake aliyefariki Dunia Machi 2021.
“Magufuli kutokana na uwezo wake kisiasa aliwafanya wakulima wa nchi hii waendelee kulima kokote wanakotaka na wauze mazao yao kokote. Tunataka Rais Samia aliyekamata kijiti chake aendelee kulinda demokrasia na hatimaye kufanya Tanzania kuishi kwa amani na utulivu.”
AAFP kinafanya mkutano wake mkuu uliobeba ajenda mbalimbali ikiwemo kujadili na kupitisha sera yake ya jinsia, kufanya marekebisho madogo ya katiba na kanuni zake.
Masuala mengine ni kuwasilisha na kuidhinisha taarifa ya utekelezaji ya 2028 hadi 2023 na uchaguzi wa viongozi kitaifa.
Kama UMEPEWA PROJECT KITAMKWACHO HAYA TUTAONANA TENA YAWEE… TUTAONANA TENA.. TUTAONANA YAWE… TUTAONANA TENA… BIBI YAKO MPYA YAWEZEKANA ALIFIKA HUKU.. Je UNATAFUTA MWANAMKE NA HAUJAOA!? NUNUA PINDA HONEY… HUYU HAPA YUPO AVAILABLE..
https://www.picuki.com/media/2040637081931345491