WAZIRI wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amesema tangu Rais, Dk. Samia Suluhu Hassan aingie madarakani, Serikali imeajiri jumla ya walimu 29,879 wa Shule za Msingi na Sekondari.
Amesema takwimu zinathibishisha mkuu huyo wa nchi anathamini kada ya walimu. Anaripoti Danson Kaijage, Kagera … (endelea).
Hata hivyo, amesisitiza Serikali itaendelea kuboresha maslahi ya walimu nchini na imedhamiria kutatua na kumaliza kero za walimu nchini ikiwa ni pamoja na madaraja na stahiki zao mbalimbali.)
Amesema hayo tarehe 27 Oktoba 2023 wilayani Karagwe mkoani Kagera katika Sherehe ya kuadhimisha kilele cha siku ya Mwalimu Duniani na miaka 30 ya Chama cha Walimu Tanzania (CWT) yenye kauli mbiu “Walimu Tuwatakao kwa Elimu Tuitakayo, Lazima Kutatua Uhaba wa Walimu”
Bashungwa amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan ambapo tangu aingie halmashauri ya wilaya Karagwe imeshapokea Sh 3.1 bilioni kuboresha elimu ya msingi na Sh 5.5 bilioni kuboresha elimu ya sekondari.
Kuhusu kanuni ya malipo ya mkupuo na malipo ya pensheni kwa wastaafu (Kikokotoo), amesema Serikali ya imeendelea kuwa sikivu na kuwathamini walimu wastaafu, na watumishi wote waliotumikiaa Taifa hili.
Leave a comment