Monday , 11 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Matumizj ya risiti, stempu feki yaitikisa TRA
Habari MchanganyikoTangulizi

Matumizj ya risiti, stempu feki yaitikisa TRA

Spread the love

MAMLAKA ya Mapato Tanzania imetoa wito kwa Watanzania kujiepusha na matumizi ya risiti na stempu feki ambazo zinaikosesha serikali mapato. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Hatua hiyo imekuja baada ya uwepo wa risiti na stempu feki ambazo nyingine hutengenezwa kutoka nje ya nchi na kuingizwa nchini kwa njia za magendo.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila akimkabidhi cheti cha shukrani Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa mlipa kodi, Richard Kayombo baada ya kuwa mmoja wa wadhamini wa mkutano mkuu wa Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Dar es Salaam(DCPC).

Akiwasilisha mada katika Mkutano Mkuu wa Waandishi wa Habari Mkoa wa Dar es Salaam(DCPC)  jana Ijumaa, Msimamizi wa masuala ya Kodi, Lucas Igembe alisema hiyo ni changamoto kubwa inayoisumbua mamlaka hiyo.

Alisema ni vema wananchi kushirikiana na mamlaka hiyo kufichua wafanyabiashara hao wasio waaminifu ili kutokomeza tabia hiyo ambayo ni sawa na utengenezaji wa fedha feki.

Aidha, Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa mlipa kodi, Richard Kayombo alisema kutokana na kukithiri kwa matumizi hayo ya stempu feku kutoka kwa wafanyabiashara wasio waaminifu, wananachi wanaweza kuhakiki stempu za bidhaa wanazonunua kuwa kupakua programu ‘Hakiki App’ inayopatikana kwenye simu rununu.

“ Pia wanaweza kupiga pichi risiti ambazo wanahisi ni feki na kuituma kwenye kitengo maalumu cha TRA kupitia namba 0744233333  kwa njia ya mtandao wa Whatsap,” alisema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Mpango: Sitakufa bali nitaishi

Spread the loveMAKAMU  wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk....

Habari Mchanganyiko

Kesi ya mfanyakazi wa CRDB itaendelea J’tatu

Spread the love  MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kinondoni, Dar es Salaam inatarajia...

Habari za SiasaTangulizi

Mbowe: Miaka 62 ya uhuru tujenge upya mioyo yetu

Spread the loveWAKATI Tanganyika ikiadhimisha miaka 62 tangu kupata uhuru, Mwenyekiti wa...

Habari Mchanganyiko

Mawasiliano Dar – Bagamoyo yarejea

Spread the loveMAWASILIANO ya barabara ya Mkoa wa Pwani na Dar es...

error: Content is protected !!