Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Matumizj ya risiti, stempu feki yaitikisa TRA
Habari MchanganyikoTangulizi

Matumizj ya risiti, stempu feki yaitikisa TRA

Spread the love

MAMLAKA ya Mapato Tanzania imetoa wito kwa Watanzania kujiepusha na matumizi ya risiti na stempu feki ambazo zinaikosesha serikali mapato. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Hatua hiyo imekuja baada ya uwepo wa risiti na stempu feki ambazo nyingine hutengenezwa kutoka nje ya nchi na kuingizwa nchini kwa njia za magendo.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila akimkabidhi cheti cha shukrani Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa mlipa kodi, Richard Kayombo baada ya kuwa mmoja wa wadhamini wa mkutano mkuu wa Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Dar es Salaam(DCPC).

Akiwasilisha mada katika Mkutano Mkuu wa Waandishi wa Habari Mkoa wa Dar es Salaam(DCPC)  jana Ijumaa, Msimamizi wa masuala ya Kodi, Lucas Igembe alisema hiyo ni changamoto kubwa inayoisumbua mamlaka hiyo.

Alisema ni vema wananchi kushirikiana na mamlaka hiyo kufichua wafanyabiashara hao wasio waaminifu ili kutokomeza tabia hiyo ambayo ni sawa na utengenezaji wa fedha feki.

Aidha, Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa mlipa kodi, Richard Kayombo alisema kutokana na kukithiri kwa matumizi hayo ya stempu feku kutoka kwa wafanyabiashara wasio waaminifu, wananachi wanaweza kuhakiki stempu za bidhaa wanazonunua kuwa kupakua programu ‘Hakiki App’ inayopatikana kwenye simu rununu.

“ Pia wanaweza kupiga pichi risiti ambazo wanahisi ni feki na kuituma kwenye kitengo maalumu cha TRA kupitia namba 0744233333  kwa njia ya mtandao wa Whatsap,” alisema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari Mchanganyiko

Dk. Jafo aipongeza Oryx kumuunga mkono Samia

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

error: Content is protected !!