Tuesday , 21 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Viongozi, Wanachama CCWT wazidi kuvutana
Habari Mchanganyiko

Viongozi, Wanachama CCWT wazidi kuvutana

Katibu wa Chama cha Wafugaji nchini, Magambe Makoye (katikati) akionesha nyaraka kwa waandishi wa habari
Spread the love

BAADHI ya wajumbe na wanachama wa Chama cha Wafugaji Tanzania (CCWT) wameendelea kuvutana na uongozi wa juu chama hicho wakitaka viongozi kuachia madaraka na kufanyika uchaguzi, anaandika Dany Tibason.

Baadhi ya madai ya wanachama na wajumbe wa chama hicho kutaka viongozi kuachia ngazi ni pamoja na kudaiwa kushindwa  kutimiza majukumu yao ikiwa ni pamoja na kushindwa kuitisha mkutano wa kusoma mapato na matumizi.

Hoja nyingine ni pamoja na kudai kwamba viongozi hao wanafanya ujanja wa kubadili kadi za uanachama wa chama hicho ikiwa ni pamoja na kubadili nembo ya awali ya chama hicho.

Mmoja wa Wenyeviti hao,Wamarwa Kusundwa alisema kuwa waliuchagua uongozi wa mpito ambao ni mwenyekiti, katibu mkuu, mtunza hazina pamoja na wajumbe 12 wa kamati tendaji mnamo mwaka 2015 kwa lengo la kutetea maslahi ya wafugaji.

“Kwa kweli tunashindwa kuuelewa uongozi huu wa sasa kwa sababu umekuwa ukijifanyia mambo kivyake bila kushirikisha kamati tendaji wala bodi ya wadhamini na mbaya zaidi hawajawahi kusoma mapato na matumizi tangu wachaguliwe,”alisema.

Katibu wa Chama cha Wafugaji nchini, Magambe Makoye hakuwa tayari kuzungumzia sakata hilo alipotakiwa kutoa ufafanuzi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tanzania yakabidhi rasmi msaada nchini Malawi

Spread the loveWAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,...

Habari Mchanganyiko

Bashe: Tumeshagawa pikipiki 5,500 kati ya 7,000 kwa maafisa ugani

Spread the love  WAZIRI wa Kilimo, Hussen Bashe, amesema wizara hiyo tayari...

Habari Mchanganyiko

Spika Tulia awapa neno mawaziri utekelezaji mashamba ya pamoja

Spread the love  SPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, amewataka mawaziri kushirikiana...

Habari Mchanganyiko

Ukosefu wa maadili kwa wakunga, wauguzi bado changamoto

Spread the loveIMEELEZWA kuwa vitendo vya uvunjifu wa maadili kwa  wauguzi na...

error: Content is protected !!