Saturday , 11 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Viongozi, Wanachama CCWT wazidi kuvutana
Habari Mchanganyiko

Viongozi, Wanachama CCWT wazidi kuvutana

Katibu wa Chama cha Wafugaji nchini, Magambe Makoye (katikati) akionesha nyaraka kwa waandishi wa habari
Spread the love

BAADHI ya wajumbe na wanachama wa Chama cha Wafugaji Tanzania (CCWT) wameendelea kuvutana na uongozi wa juu chama hicho wakitaka viongozi kuachia madaraka na kufanyika uchaguzi, anaandika Dany Tibason.

Baadhi ya madai ya wanachama na wajumbe wa chama hicho kutaka viongozi kuachia ngazi ni pamoja na kudaiwa kushindwa  kutimiza majukumu yao ikiwa ni pamoja na kushindwa kuitisha mkutano wa kusoma mapato na matumizi.

Hoja nyingine ni pamoja na kudai kwamba viongozi hao wanafanya ujanja wa kubadili kadi za uanachama wa chama hicho ikiwa ni pamoja na kubadili nembo ya awali ya chama hicho.

Mmoja wa Wenyeviti hao,Wamarwa Kusundwa alisema kuwa waliuchagua uongozi wa mpito ambao ni mwenyekiti, katibu mkuu, mtunza hazina pamoja na wajumbe 12 wa kamati tendaji mnamo mwaka 2015 kwa lengo la kutetea maslahi ya wafugaji.

“Kwa kweli tunashindwa kuuelewa uongozi huu wa sasa kwa sababu umekuwa ukijifanyia mambo kivyake bila kushirikisha kamati tendaji wala bodi ya wadhamini na mbaya zaidi hawajawahi kusoma mapato na matumizi tangu wachaguliwe,”alisema.

Katibu wa Chama cha Wafugaji nchini, Magambe Makoye hakuwa tayari kuzungumzia sakata hilo alipotakiwa kutoa ufafanuzi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC, Wizara ya Katiba wajadili uanzishaji haki binadamu katika biashara

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umefanya...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Sitta ang’ang’ana wanafunzi watibiwe bure, Serikali yagoma

Spread the loveMBUNGE wa Urambo, Margaret Sitta, ameishauri Serikali iweke utaratibu wanafunzi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Waitara ahoji bungeni mwarobaini mauaji katika mgodi Barick North Mara

Spread the loveMBUNGE wa Tarime Vijijini (CCM), Mwita Waitara, ameitaka Serikali kutafuta...

error: Content is protected !!