WAPALESTINA wawili wauawa na vikosi vya Israel kwenye matukio tofauti huko Palestina. Anaripoti Glory Massamu TUDARCo kwa msaada wa mitandao ya kimataifa … (endelea)
Mauaji hayo yametokea leo Alhamisi tarehe 30 Septemba 2021, ambapo mtu mmoja ametambuliwa kwa jina la Alaa Nasser Mohammed Zayyoud, mwenye umri wa miaka 22, kutoka katika kijiji cha Burqin na mwanamke mmoja kutokea Jerusalem.
Kwa mujibu wa ripoti za vyombo vya habari nchini humo, Zayyoud alipigwa risasi usiku katika kijiji cha burqin wakati akikabiliana kwa kutumia silaha na jeshi la Israel.
Israel ilivamia mji huo kwa kutumia gari kadhaa aina ya Jeeps za kijeshi na vikosi maalum alfajiri ya leo na kufanya shambulizi.
Wizara ya Afya ya Palestina imesema, Zayyoud alipigwa risasi nne, ambapo mbili za kifua, moja ya shingo na nyingine kwenye paja la kulia.
Mashuhuda wa tukio hilo wameviambia vyombo vya habari vya ndani kwamba sniper wa Israeli alimpiga risasi kwa karibu.
“Jeeps na jeshi likamzunguka, walizuia gari la wagonjwa kumfikia, baadaye wakaruhusu gari hilo kuja baada ya kuhakikisha kuwa amekufa,” ameyasema hayo shahidi wa tukio hilo.
Mpalestina wa pili kuuawa na majeshi ya Israel, ametambuliwa kama Israa Khuzaima mwenye umri wa miaka 30, mama wa watoto watatu, kutoka kijiji cha Qabatiya huko Jenin.
Hata hivyo, vikosi vya Israeli vimetangaza vilimpiga risasi Khuzaima kwa madai ya kwamba alijaribu kumchoma moto afisa mmoja.
Aidha, wakati operesheni za kijeshi za Israeli zikiendelea katika miji na vijiji, mashambulizi yamekua mengi kwa wakazi wa Palestina katika miezi michache iliyopita.
Agosti 2021, jeshi la Israel liliwaua Wapalestina wanne katika kambi ya wakimbizi ya Jenin wakati wa uvamizi uliosababishwa na makabiliano ya silaha.
Ambapo Jumapili tarehe 26 Septemba 2021, majeshi ya Israel yaliwaua wapalestina watano wakati wa makabiliano ya silaha kufuatia mashambulizi ya kijeshi yaliyofanywa huko Jenin na Jerusalem.
Leave a comment