Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo Vijana waadhimisha miaka 62 ya Uhuru kwa kushiriki michezo
Michezo

Vijana waadhimisha miaka 62 ya Uhuru kwa kushiriki michezo

Spread the love

UMOJA wa Vijana wa CCM (UVCCM) tawi la Mlowo, jana Jumapili wameadhimisha miaka 62 ya Uhuru wa Tanganyika kwa kuendesha michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, kuruka kamba na kukimbiza kuku huku washindi wakipata zawadi mbalimbali. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe.

Mwenyekiti wa UVCCM kata ya Mlowo, Bernad Nkwira amesema maadhimisho hayo yaliyonogeshwa na michezo hiyo ambapo waliokimbiza kuku walifanikiwa kuondoka nazo na mchezo wa mpira wa miguu mshindi alipata mbuzi.

Amesema lengo la kuendesha michezo ni kutoa hamasa kwa vijana ili wapende michezo ambapo mshindi kati ya timu ya Mji na Forest timu ya Maji ilishinda goli 3 -0 dhidi ya Forest  na kupewa zawadi ya mbuzi na timu ya Forest ikipata zawadi ya Sh 30,000.

Katibu mjumbe wa mkutano mkuu CCM mkoani Songwe, Imani Banda ameupongeza umoja huo kwa kuendesha tukio hilo kwani mbali na kuendesha michezo, wamepanda miti 3,000, kufanya harambee na kukusanya Sh milioni 1.3 za kujenga ofisi.

Ametoa rai yake kwa vijana hao kuwa ili umoja wao usonge mbele waache makundi ili wafike mbali kimaendeleo.

Diwani wa kata hiyo, Jackson Mwanda amesema tukio walilofanya vijana hao kwa kuadhimisha miaka 62 ya uhuru kwa kupanda miti, ni jambo muhimu na anajivunia kuwa na vijana wenye upeo kama huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!