Tuesday , 26 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa UVCCM yakemea vijana kuilalamikia Serikali, yawataka kugeukia kilimo, ufugaji
Habari za Siasa

UVCCM yakemea vijana kuilalamikia Serikali, yawataka kugeukia kilimo, ufugaji

Spread the love

VIJANA wa Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma wameshauriwa kuchangamkia fursa katika sekta ya kilimo, uvuvi na ufugaji ili waweze kujiajiri na kuajiri wezao badala ya kuendelea kuinyooshea vidole Serikali kwa kushindwa kuwapata ajiira. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Rai hiyo imetolewa leo tarehe 8 Septemba 2023 na Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana CCM Wilaya ya  Bahi mkoani Dodoma, Justen Sangulah alipozungumza kwenye kikao cha baraza la vijana kilichofanyika wilayani humo.

Amesema kuwa badala ya kusubiri serikali itoe ajira kwa upande wao wanatakiwa kujikita kwenye kilimo, uvuvi na ufugaji ambapo utawawezesha kujiajiri wenyewe na kuajiri vijana wezao.

Mbunge Bahi, Keneth Nollo


“Wilaya yetu ya Bahi ina sifa ya kuwepo kwa sekta mbalimbali ambazo zinazoweza kuwabadilisha vijana kimaendeleo na kiuchumi, hivyo niwaomba badala ya kusubiri ajira kutoka serikalini ni vema wakajikita kwenye fursa hizo ambazo zitawabadilisha maisha yao” amesema.

Sangulah pia amewataka vijana wa Wilaya hiyo kuiunga mkono serikali kwa juhudi zinazofanywa katika kuliletea Taifa maendeleo huku pia wakikataa kutumiwa na watu wasioitakia mema nchi hii kwa lengo la kuharibu amani.

Awali akifungua kikao cha baraza hilo la vijana Mbunge wa Bahi, Kenneth Nollo (CCM) amewataka kuungana kwa pamoja ili kuanzisha vikundi vitakavyowawezesha kupata mikopo itakayowawesha kupata miradi mbalimbali.

Amesema kuwa serikali ipo tayari kuwasimamia kwenye vikundi vitakavyoanzishwa kwa ajili ya kuhakikisha wanapata mikopo ambayo kwa upande wao itawabadilisha mitizamo ya maisha yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

Habari za SiasaTangulizi

Chande aliyeng’olewa TANESCO kwenda TTCL apelekwa Posta

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua aliyekuwa, Mkurugenzi Mkuu wa...

Habari za Siasa

Kamugisha aanika utekelezaji mpango kazi 2022/23

Spread the loveMWENYEKITI wa Ngome ya Vijana ya Chama Cha ACT-Wazalendo Mkoa...

Habari za Siasa

Vijana ACT-Wazalendo wakabidhiwa kivumbi kulinda kura uchaguzi 2024,2025

Spread the loveNGOME ya Vijana ya Chama cha  ACT-Wazalendo, imetakiwa kuwanoa wafuasi...

error: Content is protected !!