Raia nchini Urusi kuanzia leo Ijumaa wanapiga kura katika uchaguzi wa urais utakaofanyika kwa siku tatu na unaotarajiwa kumuongezea muda zaidi, Rais Vladimir Putin. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Uchaguzi huo hata hivyo, unafanyika huku kukiwa na ukandamizaji mkubwa dhidi ya upinzani, vyombo huru vya habari na makundi maarufu vya haki za binadamu na kumfungulia mlango Putin wa kuudhibiti kikamilifu mfumo wa kisiasa.
Raia wanapiga kura kwenye vituo karibu 100,000 kuanzia hii leo Ijumaa hadi Jumapili ndani ya taifa hilo na kwenye maeneo yaliyonyakuliwa na Urusi huko nchini Ukraine katikati ya vita vilivyoingia mwaka wa tatu sasa.
Waangalizi hata hivyo hawatarajii kwamba uchaguzi utakuwa huru na haki kwa kuwa wapiga kura hawana uwanja mpana wa kuchagua.
Leave a comment