Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Upinzani Sri Lanka wakutana kujadili serikali mpya
Kimataifa

Upinzani Sri Lanka wakutana kujadili serikali mpya

Waandamanaji wakiwa nje ya jengo la Ikulu ya Sri Lanka
Spread the love

 

VYAMA vya siasa vya upinzani nchini Sri Lanka vimekutana jana tarehe 10 Julai, 2022 kukubaliana kuhusu serikali mpya siku moja baada ya rais wa nchi hiyo na Waziri mkuu kutangaza kuachia madaraka. Inaripoti Mitandao ya kimataifa … (endelea).

Mbunge wa upinzani Mathiaparanan Sumathiran amesema vyama vyote vya upinzani kwa pamoja vinaweza kupata kwa urahisi wanachama 113 wanaohitajika kuonyesha wingi wa viti bungeni, ambapo watamuomba Rais wa nchi hiyo, Gotabaya Rajapaksa kutangaza serikali mpya kisha ajiuzulu.

Waziri Mkuu, Ranil Wickremesinghe amesema ataondoka madarakani baada ya serikali mpya kutangazwa jambo ambalo pia lilithibitishwa na Spika wa Bunge ambaye alisema Rajapaksa atajiuzulu Jumatano.

Waandamanaji wakiwa ndani ya Ikulu ya Sri Lanka

Shinikizo dhidi ya viongozi hao wawili lilikuwa limeongezeka baada ya mdororo wa uchumi uliosababisha uhaba mkubwa wa bidhaa muhimu, na kuwaacha watu wakitatizika kupata chakula, mafuta na mahitaji mengine.

Baada ya rais na Waziri mkuu kujiuzulu, Spika Mahinda Yapa Abeywardena atachukua usukani kama rais wa muda, kwa mujibu wa katiba ya nchi hiyo.

Waandamanaji wakiogelea katika bwawa lililopo ndani ya jengo la Ikulu ya Sri Lanka

Hayo yanajiri wakati waandamanaji wameendelea kubaki nyumbani kwa Rais Rajapaksa, na kwenye ofisi yake pamoja na makaazi ya Waziri mkuu, wakisema wataendelea kubaki hapo hadi pale viongozi hao watakapojiondoa rasmi madarakani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!