Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Ufaransa yaonywa kutoingilia kijeshi Niger
Kimataifa

Ufaransa yaonywa kutoingilia kijeshi Niger

Spread the love

Uongozi mpya wa kijeshi nchini Niger umeituhumu Ufaransa kutaka kuingilia kati kijeshi ili kumrejesha madarakani Rais aliyeng’olewa Mohammed Bazoum. Anaripoti Mariam Mudhihiri kwa msaada wa Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Hayo yanajiri wakati mivutano ikiongezeka kati ya Niger na Ufaransa, iliyokuwa mtawala wa kikoloni kwa Niger, na majirani zake.

Aidha, Waziri wa mambo ya nje wa Ufaransa, Catherine Colonna amekanusha madai hayo jana  Jumatatu jioni na kuongeza kuwa bado upo uwezekano wa kumrejesha madarakani Bazoum.

Kutokana na madai hayo, Serikali za Mali na Burkina Faso zinazoongozwa na wanajeshi nazo zilionya kwamba uingiliaji kati wowote wa kijeshi nchini Niger utachukuliwa pia kama tangazo la vita kwa nchi zao zote mbili.

Bazoum ambaye ni mshirika wa karibu wa nchi za magharibi ambaye kuchaguliwa kwake miaka miwili iliyopita kuliashiria kukabidhiana madaraka kwa njia ya amani kwa mara ya kwanza tangu uhuru wa Niger, aliondolewa madarakani tarehe 26 Julai na kiongozi wa kikosi cha ulinzi wa rais.

Mkuu huyo wa kikosi cha ulinzi wa rais, Jenerali Abdourahamane Tiani alijitangaza kuwa kiongozi, lakini madai yake yalilaaniwa kimataifa na Jumuia ya uchumi ya nchi za Afrika magharibi (ECOWAS) ambayo ilimpa wiki moja kurudisha madaraka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!